Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nilipokea taarifa za ushindi nikwa nyumbani na kwa kweli nilijawa nafuraha sana-Meja Nyaboga

Nilipokea taarifa za ushindi nikwa nyumbani na kwa kweli nilijawa nafuraha sana-Meja Nyaboga

Pakua

Chanda chema huvikwa pete walinena wahenga na hali ni kama hiyo kwa mlinda amani kutoka Kenya ambaye amechaguliwa kupokea tuzo ya Umoja wa Mataifa ya mwanajeshi mwanaharakati wa masuala ya kijinsia kwa mwaka 2020.  

Meja Steplyne Nyaboga ambaye alikuwa mshauri wa kijeshi wa masuala ya kijinsia alipohudumu katika operesheni ya Umoja wa Mataifa ya mpango wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Muungano wa Afrika wa kulinda amani Darfur (UNAMID) katika mahojiano maalum na Grace Kaneiya akiwa huko Nairobi Kenya amesema alipokea habari za ushindi, “kwa furaha isiyo kifani” 

Audio Credit
Leah Mushi/Grace Kaneiya
Audio Duration
3'43"
Photo Credit
UN/UNIC Nairobi