Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Pete Muller for the ICC

Wanawake Uganda wataka haki ya ardhi kwa kurekebisha sheria ya ndoa na talaka.

Lengo namba 5 la Malengo ya Umoja w mataifa ya maendeleo endelevu linaangazia usawa wa kijinsia likilenga kufanya mageuzi ili kuwapa wanawake haki sawa kwa rasilimali za kiuchumi, na pia kupata umiliki na udhibiti wa ardhi na aina nyingine za mali, huduma za kifedha, urithi na maliasili, kwa mujibu wa sheria za kitaifa. 

Mojawapo ya viashiria vya kufanikiwa kwa lengo hilo ni pale ambapo kutakuwa na uwiano wa nchi ambazo mfumo wa kisheria (pamoja na sheria ya kimila) unahakikishia haki sawa za wanawake kwa umiliki wa ardhi na au udhibiti. 

Sauti
4'10"
UN/ Jason Nyakundi

Vijana waunda roboti ya kusaidia watu wenye ulemavu

Hawana kisomo cha chuo kuu lakini ujuzi wao katika masuala ya teknolojia ya kuunda roboti inayoweza kusoma na kuelewa anachofikria mwanadamu na ni uvumbuzi ambao umewashangaza wengi. Moses Njoroge na David Gathu ni wavumbuzi walio na karakana yao ndogo eneo la Kikuyu kaunti ya Kiambu nje kidogo ya mji wa Nairobi nchini Kenya, ambapo kwa kipindi cha miaka 10 wamejikita katika kuunda roboti inayoweza kuwasaidia watu walio na ulemavu wa miguu na mikono kujihudumia. Mwandishi wetu nchini Kenya Jason Nyakundi amezungumza nao akianza na Moses.
 

Sauti
4'35"
UN/ John Kibego

Lugha yamkosesha kazi kijana mkimbizi wa DRC nchini Uganda

Vijana wakimbizi hukumbwa na changamoto nyingi ukimbizini hususan kipato kutokana na kutokuwa na ajira ambapo mara nyingine badhi yao wamejikuta katika mikono isiyo salma katika jamii za wenyeji na hata zile za wakimbizi wenzao.

Mengi hutokea wakati wanaposaka kipato ili kijikimu na kusaida jamaa zao wakisaka riziki zao katika miji iliyo karibu.

Mfano wa hivi kairbuni ni kijana Mary Furaha ambaye amejikuta katika mji wa Hoima nchini Uganda akisaka ajira ya kuela watoto nyumbani lakini kilichozua tatizo ni lugha ya kuzungumza na wajiri na watoto wao. 

Sauti
3'40"
UN/Eskinder Debebe

HER AFRICA yajitoa kimasomaso kuelimisha kuhusu hedhi salama

Suala la hedhi salama na elimu ya kifedha yamekuwa ni mambo ambayo kwa kiasi kikubwa yana mkwamo kwa watoto wa kike hususan katika nchi zinazoendelea. Kupata taulo za kike ni changamoto kubwa na hivyo kusababisha mtoto wa kike ambaye tayari amebalehe kushindwa kwenda shuleni kwa kipindi chote cha hedhi kila mwezi. Hii ni moja ya sababu zinazokwamisha lengo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDG kuhusu usawa wa kijinsia.

Sauti
3'57"
UN/ John Kibego

Vijana wa kike wahimizwa kupigania haki za kumiliki ardhi Uganda.

Wiki hii dunia ikiwa imeadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake duniani ambapo sehemu mbalimbali wanawake waliitumia kuonesha kero zao na kutiana moyo. Nchini Uganda, wanawake katika wilaya ya Buliisa wameandamana hadi Makao Makuu ya wilaya hiyo kuwasilisha malalamiko yao wakiitaka serikali ishughulikie changamoto yao ya kunyimwa haki ya kumiliki ardhi.

Sauti
3'51"
UN Tanzania

Mpango wa 'He for She' umeniwezeshakutambua changamoto zinazomkabili mtoto wa kike - Paul Siniga.

He for She ni juhudi za ulimwengu kupitia umoja wa Mataifa, kutaka kuwashirikisha wanaume na wavulana katika kufikia usawa wa kijinsia na kuchukua hatua dhidi ya mtazamo mbaya kuhusu jinsia. Paul Siniga ni kijana mwanaharakati na Balozi wa Malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs ambaye anajikita na lengo namba 5 linalohamasisha usawa wa kijinsia.

Sauti
2'35"
UN/Ahimidiwe Olotu

Tunajivunia kwamba watu wajitoleao katika Umoja wa Mataifa, wanachangia utimizaji wa SDGs

Ni takribani miaka 50 tangu Baraza la Umoja wa Mataifa lilipopitisha uanzishwaji wa mradi wa kujitolea wa Umoja wa Mataifa. Katika kipindi chote hicho, watu wenye utaalamu mbalimbali wamechangia katika shughuli mbalimbali za Umoja wa Mataifa kote duniani. Christian Mwamanga ni Mratibu wa mradi katika nchi ya Tanzania, kupitia mahojiano haya yaliyofanywa na Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam, anaeleza jinsi ambavyo mradi na watu wajitoleao, wamekuwa sehemu ya utimizaji wa malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu. 

Sauti
3'29"
UN/ John Kibego

Mabadiliko ya tabianchi yameacha kovu kwa wenyeji wa Ziwa Albert, Uganda.

Mafuriko makubwa ambayo yanayohusishwa na mabadiliko ya tabianchi, yameshuhudiwa katika meneo mengi duniani kote na yamekuwa yakiathiri watu kwa namna tofauti. Sudan, Sudan kusini, Uganda na India ni miongoni mwa nchi zilizoathirika na hali hii hususani katika kipindi cha kuelekea mwishoni mwa mwaka jana wa 2020. Ili kufuatilia maisha ya walioathirika na hali hii, mwandishi wetu wa Uganda John Kibego, amezungumza na Nyanjura Nyangoma mwanamke anayelea familia ya watoto 14 pembezoni mwa Ziwa Albert.

Sauti
3'49"
Photo FAO/Marco Salustro

Matunda ni lishe muhimu katika mlo wa kila siku

Emmanuel Mwanjisi ni Afisa lishe kutoka hospitali ya Consolatha, Ikonda, katika wilaya ya Makete, nyada za juu kusini mwa Tanzania, akieleza faida za ulaji wa mbogamboga na matunda katika mwili wa binadamu ameeleza kuwa wataalamu wa lishe wanapohamasisha ulaji wa matunda hawamaanishi kuwa ni lazima mlaji ale kiasi kikubwa cha matunda hayo bali kiasi chochote hata kipande kidogo lakini mara kwa mara, kinasaidia kuleta faida mwilini. 

Audio Duration
3'50"
© FAO-Magnum Photos/Alex Webb

Wengi wetu hatukamilishi makundi yote matano ya chakula-Afisa Lishe Mwanjisi.

Emmanuel Mwanjisi ni Afisa lishe kutoka hospitali ya Consolatha, Ikonda, katika wilaya ya Makete, nyada za juu kusini mwa Tanzania, anaeleza faida za ulaji wa mbogamboga na matunda katika mwili wa binadamu ikiwemo kuimarisha kinga za mwili. 

Bwana Emmanuel anaeleza kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakila milo ambayo haizingatii makundi matano ya chakula, na mara nyingi makundi ya mbogambona na matunda ndio yanayoondolewa katika mpangilio wa vyakula na matokeo yake kutetereka kwa afya za wanadamu.