Wanawake Uganda wataka haki ya ardhi kwa kurekebisha sheria ya ndoa na talaka.
Lengo namba 5 la Malengo ya Umoja w mataifa ya maendeleo endelevu linaangazia usawa wa kijinsia likilenga kufanya mageuzi ili kuwapa wanawake haki sawa kwa rasilimali za kiuchumi, na pia kupata umiliki na udhibiti wa ardhi na aina nyingine za mali, huduma za kifedha, urithi na maliasili, kwa mujibu wa sheria za kitaifa.
Mojawapo ya viashiria vya kufanikiwa kwa lengo hilo ni pale ambapo kutakuwa na uwiano wa nchi ambazo mfumo wa kisheria (pamoja na sheria ya kimila) unahakikishia haki sawa za wanawake kwa umiliki wa ardhi na au udhibiti.