Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano

Katika vita vya ukimwi Tanzania kuongeza elimu, madawa na utafiti:Dr Bilal

Serikali ya Tanzania inasema pamoja na kupiga hatua katika vita dhidi ya ukiwmi bado ina safari ndefu ingawa zaidi ya asilimia 50 ya waathirika wanapata dawa za kurefusha maisha.

Kwa mujibu wa Makamu wa Rais wa nchi hiyo Dr Mohammed Gharib Bilal aliyezungumza kwa kina na mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa mataifa Flora Nducha nia yao ni kufikia maambukizi sufuri, vifo sufuri na unyanyapaa sufuri dhidi ya ukimwi.

Ingawa bado ina changamoto Kenya inasema imepiga hatua katika vita vya ukimwi

Pamoja na kwamba mkutano wa ngazi ya kimataifa wa ukimwi ulioandaliwa na Umoja wa Mataifa umekamilika lakini vita dhidi ya ukimwi vinaendelea.

Viongozina wawakilishi 3000 kutoka nchi zaidi ya 30 waliokuwa wakikutana wametoka na azimio la kuweka malengo ikiwa ni pamoja na kupunguza kwa asilimia 50 HIV ifikapo 2015, pia wanadhamiria kupunguza kwa nusu maambukizi ya HIV kwa wanaotumia mihadarati na kuhakikisha kwamba ahakuna mtoto atakayezaliwa na virusi vya HIV.

UM umezindua mpango kukabiliana na unyanyapaa kwa wenye HIV

Umoja wa Mataifa leo Juni 8 umezindua mpango maalumu wa kukabiliana na unyanyapaa kwa wafanyakazi wanaoishi na virusi vya HIV katika mada ya “unyanyapaa unachagiza maambukizi zaidi”.

Kampeni hiyo pamoja na kuzinduliwa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York ambako wakuu wan chi na wawalikishi kutaoka mataifa zaidi ya 30 wanakutana kwa siku tatu kujadili hatua zilizopigwa na zipi mpya zichukuliwe katika vita vya ukimwi pia imezinduliwa katika ofisi mbalimbali za Umoja wa Mataifa kote duniani.

Gharama za matibabu katika nchi zinazoendelea ni changamoto:UM

Gharama ya matibabu hasa katika mataifa yanayostawi imetajwa kama changamoto kubwa katika vita dhidi ya magonjwa.

Kukabiliana na magongwa ni miongoni mwa malengo ya maendeleo ya milenia yaliyoainishwa na Umoja wa Mataifa baada ya wakuu wa nchi kuyapitisha mwaka 200, lakini imebainika kuwa watu wanaoishi katika umaskini wanaendelea kulemewa na mzigo wa kugharamia matibabu.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa bima ya matibabu  ni muhimu lakini sio mataifa yoye yanayomudu kuhakikisha hilo kwa watu wake.

Shirika la kimataifa la uhamiaji linasaidia watu wanaokimbia machafuko Abyei

Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan umesema wakati maelfu ya watu wakikimbia jimbo la Abyei Sudan kutokana na machafuko na kuelekea Sudan Kusini, mashirika ya misaada yanaongeza juhudi za msaada wa kibinadamu.

Jumbe Omari Jumbe , msemaji wa Shirika la kimataifa la uhamiaji (IOM) amezungumza na Redio ya Umoja wa Mataifa hii leo juu ya hali katika eneo la Abyei na juhudi za IOM kuwasaidia wale wanaokimbia  machafuko jimbo hilo la Sudan.

Serikalia ya mpito ya Somalia lazima iafikiane:UM

Serikali ya mpito ya Somalia imeambiwa sasa umefika wakati wa kumaliza tofauti zao, na kuzingatia maslahi ya taifa.

Wito huo umetolewa na ujumbe wa braza la usalama la Umoja wa mataifa uliohitimisha mkutano wa kujadili hali ya Somalia mjini Nairobi Kenya.

Ujumbe huo umetoa muda wa wiki kadhaa hadi katikati ya Juni kwa Somalia kufikiri, kujadili na kuamua hatma ya taifa lao kwa kuitisha uchaguzi na kumaliza kipindi cha mpito kama ilivyopangwa.

IOM kusafirisha mamia ya wahamiaji waliokwama jangwani Chad

Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM kuanzia mwishoni mwa wiki hii wataanza kuwasafirisha maelfu ya wahamiaji waliokwama jangwani mpakani mwa Chad na Niger.

Wahamiaji hao ni wale wanaokimbia machafuko Libya, na kujikuta wamekwama kwa kukosa urafiri wa kuwafikisha Chad. Kwa mujibu wa IOM wahamiaji hao wengi kutoka Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara watasafirishwa kwa njia ya malori na watakuwa na safari ngumu na ndefu ya zaidi ya siku 20 jangwani.

Suluhu ya Somalia ni kutekeleza muafaka wa kisiasa na kufanya uchaguzi:Mahiga

Somalia ambayo kwa zaidi ya miongo miwili sasa haina serikali kuu inazidi kujikuta katika njia panda ya kisiasa kwa mgawanyiko kughubika uhusiano baina ya Rais wa serikali ya mpito na spika wa bunge.

Kwa mujibu wa mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa Somalia balozi Agustine Mahiga tofauti hizo zinazidisha adha kwa mamilioni ya wasomali waliochoka vita na wenye kiu ya amani ya kudumu.

Hali ya Wachad wanaokimbia machafuko Libya yanatia hofu:IOM

Shirika la kimataifa la uhamaijai IOM linasema kuwa maelfu ya watu wanazidi kukimbia mzozo nchini Libya kila siku huku wasiwasi ukiibuka kuhusu hali ya raia wa Chad wanaowasili kwenye miji ya jangwani ya Faya na Kalait.

Jumbe Omari Jumbe msemaji wa shirika hilo la IOM anafanua zaidi alipozungumza na Alice Kariuki wa Idhaa hii

(MAHOJIANO NA JUMBE OMARI JUMBE)

Kenya yaliandikia baraza la usalama ikitaka kesi dhidi ya wakenya sita huko ICC zihairishwe kwa mwaka mmoja

Akizungumza na mkuu wa Idhaa ya Radio ya Umoja wa Mataifa Flora Nducha, balozi wa Kenya kwenye Umoja wa Mataifa Macharia Kamau amesema wanachotaka sio kwamba kesi zifutwe zinazowakabilia maafisa sita wa zamani wa serikali ambao ni Uhuru Kenyatta naibu waziri mkuu, Henry Kosgei, Mohammed Hussein Ali aliyekuwa mkuu wa polisi, William Ruto, Francis Muthaura, na mwandishi habari Joshua Arap sang  bali ziahirishwe kwa mwaka mmoja hadi baada ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Amesema zikiendelea sasa zinaweza kuleta chuki na mgawanyiko mkubwa wakati kampeni za uchaguzi mkuu ujao zi