Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

21 NOVEMBA 2022

Hii leo jarida linaangazia siku ya uvuvi, masuala ya watoto na makala tunakwenda nchini Somalia kumulika uhakika wa chakula kwa watu waliokumbwa na changamoto ya ukame na mafuriko, mashinani ni ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Sauti
12'29"

18 NOVEMBA 2022

Hii leo jarida linaangazia ripoti iliyotolewa leo na UNICEF kuhusu ubaguzi wa rangi na ubaguzi dhidi ya watoto na pia habari kutoka Garissa, Kenya, makala ya maandamanano ya wanaharakati huko Sharm-el-Sheikh nchini Misri kwenye mkutano wa 27 wa nchi wanachama wa Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi, COP27, kisha mashinani nchini Ethiopia.

Sauti
12'15"

17 NOVEMBA 2022

Hii leo jaridani tunaangazia mada kwa kina na leo tunafunga safari hadi bara Hindi huko nchini India kusikia kuhusu kijiji cha kwanza nchini humo kinachotumia nishati ya sola pekee kwa wakazi wake zaidi ya 6,400.  Pia litakuletea Habari kwa ufupi kama zifuatayo:

Sauti
12'23"

16 Novemba 2022

Hii leo jaridani tunaangazia mabadiliko ya tabianchi na athari kwa wakimbizi, ziara ya afisa wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan, Makala tunamulika haki za wenye ualbino Uganda na mashinani tunamulika nafasi ya wananawake kwenye maamuzi.

Sauti
13'28"

15 NOVEMBA 2022

Leo katika Jarida la Habari za Umoja wa Mataifa tunakuletea Habari kwa Ufupi zikimulika idadi ya watu kufikia bilioni 8, Mada kwa Kina tunakupeleka Peru kumulika wanawake wa jamii ya asili na upandaji miti, na Mashinani tunamulika polisi wa Umoja wa Mataifa na ulinzi wa amani.

1. Habari Kwa Ufupi:

Sauti
12'12"

14 NOVEMBA 2022

Hii leo katika Habari za UN mwenyeji wako akiwa Assumpta Massoi tunamulika ugonjwa wa kisukari barani Afrika, jawabu la nishati salama Malawi, vijana na wito wao huko Sharm el- sHeikh kwenye COP27 na ujumbe wa Balozi mwema wa IFAD Sabrina Dhowre Elba.

1. Wakati dunia ikiadhimisha hii leo siku ya kisukari duniani kwa lengo la kuelimisha umma kuhusu ongezeko la mzigo wa ugonjwa huo na mikakati ya kuzuia na kudhibiti tishio lake, bara la Afrika linaonekana kuwa na changamoto kubwa ya ugonjwa huo, kwa mujibu wa takwimu za shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO. 

Sauti
13'4"

10 NOVEMBA 2022

Katika Jarida la habari la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea 

-Huko Sharm el Sheikh kwenye mkutno wa COP27 vijana watoa wito kwa nchi wachafuzi wa mazingira kugharamia hasara na uharibifu wa janga hilo

-Nchini Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo DRC ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO washikana na jeshi la serikali FARDC kuendesha doria kulinda raia

-Nchini Lebanon shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na wadau wa chanjo wafikisha chanjo 600,000 kwa ajili ya kampeni dhidi ya kipindupindu itakayoanza Jumamosi

Sauti
13'40"

09 NOVEMBA 2022

Karibu katika jarida la Habari za UN hii leo ambalo kwa kiasi kikubwa linamulika harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na wakati huo huo hatua za kuchukua wakati huu ambapo mabadiliko ya tabianchi yanaathiri jamii mbalimbali duniani.

Sauti
13'13"

08 NOVEMBA 2022

Hii leo katika Habari za UN tunakuletea Habari kwa Ufupi, Mada kwa Kina na Mashinani na zote zikiwa ne mrengo wa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi unaofanyika huko Sharm el-Sheikh nchini Misri.

Sauti
10'38"