13 DESEMBA 2022
Jaridani leo tunakuletea mada kwa kina tukimulika mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu mkataba wa kimataifa wa bayoanuai CBD unaoendelea mjini Montreal Canada. Pia tunakuletea habari kwa ufupi kutoka huko huko Montreal Canada, nchini Somalia na nchini Haiti. Mashinani tunakuletea ujumbe wa mwanauchumi mashuhuri duniani Sir Partha Dasgupta, anasemaje?