10 NOVEMBA 2022
Katika Jarida la habari la Umoja wa Mataifa hii leo Assumpta Massoi anakuletea
-Huko Sharm el Sheikh kwenye mkutno wa COP27 vijana watoa wito kwa nchi wachafuzi wa mazingira kugharamia hasara na uharibifu wa janga hilo
-Nchini Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo DRC ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO washikana na jeshi la serikali FARDC kuendesha doria kulinda raia
-Nchini Lebanon shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na wadau wa chanjo wafikisha chanjo 600,000 kwa ajili ya kampeni dhidi ya kipindupindu itakayoanza Jumamosi
-Mada yetu kwa kina inatupeleka COP27 Sharm el Sheikh Misri ambapo leo utasikia sauti mbalimbali kutoka kwa viongozi wa kisiasa, jamii za asili na vijana
-Na katika kujifunza Kiswahili tunabisha hodi Tanzania Baraza la Kiswahili la Taifa BAKITA kupata ufafanuzi wa neno MUKU