Ziara ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Barani Afrika!
Wiki hii Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amezuru barani Afrika akianzia Ukanda wa Maziwa Makuu ambapo ametembelea Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya congo DRC na hatimaye akaelekea Sudan Kusini ambako kwenye nchi hizo tatu amemulika umuhimu wa kukuza amani na demokrasia kupitia mazungumzo jumuishi ya kisiasa.