Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Jamii ya kimataifa ni lazima itimize wajibu wa kulinda raia- Eliasson

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jan Eliasson, ametoa wito kwa jamii ya kimataifa ithibitishe wajibu wake wa kulinda raia, kama ilivyo weka ahadi katika mkutano wa mwaka 2005.

Bwana Eliasson amesema hayo akilihutubia jopo la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ambalo limekutana kujadili kuhusu utekelezaji wa dhamira ya wajibu wa kulinda, miaka kumi tangu dhana hiyo ilipoanzishwa kwenye mkutano wa kimataifa.

Akihoji hatua zilizopigwa miaka kumi tangu ahadi hiyo kuwekwa, Bwana Eliasson ameuliza

Wagombea nafasi ya ukatibu mkuu UM kujieleza mbele ya Baraza Kuu

Mchakato wa kupata Katibu Mkuu wa Tisa wa Umoja wa Mataifa unaendelea kushika kasi ambapo hii leo Rais wa Baraza Kuu la umoja huo Mogens Lykettoft ametangaza kufanyika kwa mazungumzo yasiyo rasmi ya kuwasikiliza wagombea kama moja ya njia ya kuweka uwazi katika mchakato huo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani Bwana Lyketofft amesema hadi sasa wamepokea rasmi majina sita ya wagombea ambapo watatu ni wanawake na watatu ni wanaume na kuna tovuti maalum kwa wagombea hao.

Raia walindwe, misaada iwafikie wahitaji Sudan Kusini: Kyung-wha Kang

Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya kibinadamu Kyung-wha Kang, leo amehitimisha zaiara yake ya siku mbili nchini Sudan Kusini akitaka pande kinzani kulinda raia na kuruhusu bila vikwazo ufikishwaji wa misaada ya kibinadamu.

Kiongozi huyo ambaye aliambatana na Katibu Mkuu Ban Ki-moon katika ziara hiyo ambapo walikutana na maafisa wa serikali na kutembelea jamii zilizoathirika kutokana na machafuko.

Marais watano wa Afrika watua Burundi kusaka suluhu

Ujumbe wa Marais watano wa Afrika umewasili Burundi hii leo katika  jitihada za  kujaribu  kutanzua mgogoro wa kisiasa nchini humo uliodumu zaidi ya miezi kumi  na kushuhudia mauaji  ya watu zaidi 400 huku zaidi ya  raia laki mbili unusu wakilazimika kutoroka  nchi na  kuchukua  hifadhi katika chi jirani. Katibu Mkuu wa Umoja wa  Mataifa Ban Ki Moon alikuwa Burundi wiki hii na kuhakikishiwa na serikali  azma yake ya kuanzisha mazungumzo jumuishi. Kutoka bujumbura, mwandishi wetu Ramadhani KIBUGA anasimulia zaidi.

Akiwa DRC, Katibu Mkuu awaambia viongozi kuachia madaraka

Mapema kabla hajaelekea nchini Sudan Kusini,  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewasihi viongozi wa kisaisa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kushiriki mazungumzo jumuishi ya kisiasa kuelekea uchaguzi mwaka huu, na kuheshimu katiba.

Bwana Ban amesema hayo akizungumza na waandishi wa habari mjini Kinshasa, mwisho wa ziara yake nchini DRC, akieleza wasiwasi wake kuhusu kuchelewa kwa ajenda ya uchaguzi na ripoti za vikwazo dhidi ya vyombo vya habari, asasi za kiraia na vyombo vya upinzani.

Makubaliano ya polisi Ulaya yaweka wakimbizi hatarini: Zeid

Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu katika Umoja wa Mataifa Zeid Ra' ad Al Hussein ameelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusu harakati za kiusalama zilizochukuliwa na wakuu wa polisi wa nchi tano za ulaya, akisema zitakuwa na madhara mabaya kwa haki za binadamu za wakimbizi na wahamiaji kwenye ukanda wa Ulaya mashariki na Kusini.

Kwenye taarifa iliyotolewa leo Kamishna Zeid amesema  tayari baadhi ya wakimbizi na wahamiaji wameanza kufukuzwa kwenye njia inayopitia Austria, Slovenia, Croatia, Serbia na Macedonia.

WHO yatoa muongozo kuhusu dalili, na unyonyeshaji kwa watoto wenye virusi vya Zika

Shirika la afya ulimwenguni WHO leo limechapisha nyaraka tatu zenye miongozo kuhusu mambo matatu katika kukabiliana na virusi vya Zika  ambayo ni tathmini ya watoto wachanga wenye vichwa vidogo, utambuzi na uongozi dhidi ya dalili na unyonyeshaji wa watoto.

Katika machapisho hayo WHO imetahadharisha jamii kuwa watoto wanaozaliwa na vichwa vidogo hutambulika kutokana na kudumaa katika hatua za ukuaji mathalani uwezo wao wa kiakili, hukumbwa na degedege, na hata ulemavu wa viungo ikwamo kutosikia na kutoona.

Haki ya Miji Salama na Safi bado ni chagamoto Kenya

Haki za Binadamu, ikiwa ni pamoja na haki ya nyumba za kutosha, maji safi na salama na usafi wa mazingira ni miongoni mwa haki zilizomo katika Azimio la Kimataifa la Haki za Binadamu na mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na Mkataba wa Kimataifa wa Uchumi, Jamii na Utamaduni ambazo zimeridhiwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa.