Watoto 60,000 wanakabiliwa na kifo Somalia
Takribani watoto 60,000 wanakabiliwa na kifo nchini Somalia kwa sababu ya kukosa msaada , kwa mujibu wa mratibu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya kibinadamu kwenye nchi hiyo ya pembe ya Afrika.
Mtafaruku wa kisiasa, kurejea mara kwa mara kwa ukame na hata mafuriko, inamaanisha kwamba watoto wapatao milioni tano au nusu ya watu wote wa Somalia wanahitaji aina fulani ya msaada.
Umoja wa mataifa unasema, unahitaji dola takribani milioni 900 kwa ajili ya shughuli za msaada, lakini hadi sasa imepokea asilimia mbili tuu ya fedha hizo.