Wagombea nafasi ya ukatibu mkuu UM kujieleza mbele ya Baraza Kuu
Mchakato wa kupata Katibu Mkuu wa Tisa wa Umoja wa Mataifa unaendelea kushika kasi ambapo hii leo Rais wa Baraza Kuu la umoja huo Mogens Lykettoft ametangaza kufanyika kwa mazungumzo yasiyo rasmi ya kuwasikiliza wagombea kama moja ya njia ya kuweka uwazi katika mchakato huo.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani Bwana Lyketofft amesema hadi sasa wamepokea rasmi majina sita ya wagombea ambapo watatu ni wanawake na watatu ni wanaume na kuna tovuti maalum kwa wagombea hao.