Ethiopia yakumbwa na ukame mkali, WFP yatoa wito kwa ufadhili
Nchini Ethiopia, mahitaji ya kibinadamu yameongezeka mara tatu tangu mwanzo wa mwaka 2015 kutokana na ukame mkali unaokumba baadhi ya maeneo ya nchi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula WFP limesema El-Nino ambayo mwaka huu imekuwa mbaya zaidi imehatarisha zaidi hali hiyo na kusababisha mazao kuharibika, na mifugo kufa kwa wingi, huku utapiamlo wa kupindukia ukiathiri nusu ya wilaya za Ethiopia.