Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Mtoto mwenye umri wa mwaka 1 anafanyiwa unchunguzi wa matibabu kama kuna dalili za utapiamlo katika kituo cha mapokezi kwenye mpaka wa Sudan na Sudan Kusini.
© WFP/Hugh Rutherford

Uongozi wa jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini waomba usaidizi zaidi wa ulinzi

Huku mzozo wa Sudan ukiendelea, wakimbizi na wanaorejea wanamiminika katika mipaka ya nchi jirani ya Sudan Kusini, wengi wamekuwa wakitafuta hifadhi katika jimbo la Upper Nile nchini humo na wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.  Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umefanya mazungumzo na uongozi wa jimbo hilo kuona namna ya kuwasaidia.

Sauti
2'25"
Familia ya wakimbizi wa Sudan Kusini wanaorejea wakisubiri katika kituo cha UNHCR cha Renk, Sudan Kusini. (Maktaba)
© UNHCR/Andrew McConnell

UNHCR na Benki ya Maendeleo ya Afrika waungana kusaidia wakimbizi nchini Sudan Kusini

Vita vinapotokea wananchi wanalazimika kusaka kila namna ya kujilinda na kuokoa maisha yao. Mambo yanapokuwa mabaya watu hao hulazimika kuacha kila kitu nyuma na kukimbia kwenda kusaka hifadhi sehemu nyingine. Watu hao wanapoondoka wanaondoka na ujuzi wao mfano kama alikuwa muuguzi, mfanya biashara, fundi muashi au taaluma yoyote ile. 

Sauti
3'47"