Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Ukame huu nchini Kenya, haujawahi kutokea na sio janga la asili, tuwasaidie
Umoja wa Mataifa na wadau wake wa masuala ya kibinadamu nchini Kenya wameomba dola milioni 472.6 kusaidia watu milioni 4.3 walioathiriwa na ukame mwaka wa 2023, ili kuunga mkono mwitikio unaoongozwa na Serikali, huku janga hilo likitarajiwa kuwa mbaya zaidi.
COP27 ikielekea ukingoni Guterres amewataka wajumbe kuzingatia hasara na uharibifu
Mkutano wa 27 wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi utafungwa angalau siku moja baadaye kuliko ilivyotarajiwa, ofisi ya Rais wa Misri imetangaza leo Ijumaa, ikitoa wito kwa wajadili kubadili msimamo ili makubaliano yaweze kufikiwa kuhusu mambo yaliyosalia yanayohitaji mshikamano.
Kisima kinachotumia nishati ya jua chawa mkombozi wa elimu kijijini Daley, Garissa, Kenya
Msaada wa kisima cha maji uliofanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika shule ya Msingi ya Daley kwenye Kijiji cha Daley, Kaunti ya Garissa nchini Kenya, umesaidia sana jamii hasa katika suala la elimu katika eneo hilo la nchi ambayo imekosa mvua ya kutosha kwa misimu mitano mfululizo.
Mustakbali wetu umeporwa ni wakati wa kushughulikia hasara na gharama:Vijana COP27
Wakiwa wamebeba mabango, vibao vyenye ujumbe, spika, na hasa kwa wakitoa ujumbe wenye kugusa moyo unaoungwa mkono na ukweli wa kisayansi na kiuchumi, vijana leo wametawala kumbi za COP27 wakiwataka viongozi wajadili jinsi ya kushughulikia suala la hasara na uharibifu utokanao na mabadiliko ya tabianchi.
Sekta ya ujenzi yaenda kombo katika kutozalisha kabisa hewa ukaa ifikapo 2050:UNEP Ripoti
Kushamiri kwa sekta ujenzi kimataifa kumesukuma uzalishaji wa hewa ukaa au CO2 wa sekta hiyo hadi kiwango cha juu cha gigatani 10, ikimaanisha kuwa sasa sekta hilo imekwenda kombo haijafanikiwa kufikia ahadi za utokomezaji wa hewa ukaa ifikapo mwaka 2050, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira (UNEP).
COP27 yafungua pazia, ni ukurasa mpya wa kufanya mambo tofauti :UNFCCC
Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP27 umefungua pazia leo huko Sharm el-Sheik, Misri, na unapaswa kuuelekeza ulimwengu kwenye utekelezaji wa mipango iliyokubaliwa hapo awali ya kukabiliana na changamoto kubwa za ubinadamu, amesema wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Simon Stiell, katibu mtendaji mpya wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi wa Umoja wa Mataifa (UNFCCC).
Ripoti mpya ya mabadiliko ya tabianchi ni historia ya zahma kubwa: UN
Ripoti mpya ya shirika la utabiri wa hali ya hewa la Umoja wa Mataifa WMO, iliyotolewa leo Jumapili, inaonyesha kuwa miaka minane iliyopita imekuwa ya joto zaidi katika historia ya rekodi, ikichochewa na kuongezeka kwa viwango vya gesi chafuzi.
Afya lazima iwe kitovu katika majadiliano ya mabadiliko ya tabianchi COP27: WHO
Katika mkesha wa mazungumzo muhimu ya mabadiliko ya tabianchi COP27, yanayoanza kesho huko Sharm-el Sheikh nchini Misri, shirika la afya la Umoja wa Mataifa Ulimwenguni WHO, limekumbusha kwamba mzozo wa mabadiliko ya tabianchi unaendelea kuwafanya watu kuwa wagonjwa na kuhatarisha maisha na kwamba afya lazima iwe msingi wa mazungumzo haya muhimu.
Tahadhari ya mapema inaokoa maisha wakati wa Tsunami:UNDRR
Tsunami inaweza kuwa moja ya hatari mbaya zaidi na inayokatili maisha ya watu wengi amesema mwakilishi wa Katibu Mkuu na mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya upunguzaji hatari za majanga UNDRR Mami Mizutori.
Mabadiliko ya tabianchi yanaweza kuwa mbaya kama saratani katika baadhi ya nchi duniani: UNDP
Bila hatua za pamoja na za haraka, mabadiliko ya tabianchi yatazidisha ukosefu wa usawa na kupanua pengo katika maendeleo ya binadamu kulingana na jukwaa jipya lililopewa jina “Human Climate Horizons” lililozinduliwa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP na maabara ya athari za mabadiliko ya tabianchi.