Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Tarehe 26 Oktoba 2022, katika kijiji cha Daley katika Kaunti ya Garissa, Kenya - (kutoka kushoto kwenda kulia) Osman (11), Abdullahi (15) na Abdi (12) wa shule ya msingi ya Daley wakinywa maji safi na salama yanayotoka katika kisima kinachoendeshwa kwa n…
©UNICEF/James Ekwam

Kisima kinachotumia nishati ya jua chawa mkombozi wa elimu kijijini Daley, Garissa, Kenya

Msaada wa kisima cha maji uliofanikishwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF katika shule ya Msingi ya Daley kwenye Kijiji cha Daley, Kaunti ya Garissa nchini Kenya, umesaidia sana jamii hasa katika suala la elimu katika eneo hilo la nchi ambayo imekosa mvua ya kutosha kwa misimu mitano mfululizo.

Sauti
3'14"
Simon Stiell mkuu wa UNFCCC akizungumza katika ufunguzi wa COP27
UN Japan/Momoko Sato

COP27 yafungua pazia, ni ukurasa mpya wa kufanya mambo tofauti :UNFCCC

Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP27 umefungua pazia leo huko Sharm el-Sheik, Misri, na unapaswa kuuelekeza ulimwengu kwenye utekelezaji wa mipango iliyokubaliwa hapo awali ya kukabiliana na changamoto kubwa za ubinadamu, amesema wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Simon Stiell, katibu mtendaji mpya wa mkataba wa mabadiliko ya tabianchi wa Umoja wa Mataifa (UNFCCC).

Mwanamke akijarivu kuvuka maji ya mafuriko mjini Jakusko jimbo la Yobe Nigeria
© WFP/Arete/Ozavogu Abdul

Afya lazima iwe kitovu katika majadiliano ya mabadiliko ya tabianchi COP27: WHO

Katika mkesha wa mazungumzo muhimu ya mabadiliko ya tabianchi COP27, yanayoanza kesho huko Sharm-el Sheikh nchini Misri, shirika la afya la Umoja wa Mataifa Ulimwenguni WHO, limekumbusha kwamba mzozo wa mabadiliko ya tabianchi unaendelea kuwafanya watu kuwa wagonjwa na kuhatarisha maisha na kwamba afya lazima iwe msingi wa mazungumzo haya muhimu.

Mafuta kisukuku yanachangia uchafuzi wa hewa ambao unaathiri mazingira na binadamu
© Unsplash/Juniper Photon

Mabadiliko ya tabianchi yanaweza kuwa mbaya kama saratani katika baadhi ya nchi duniani: UNDP 

Bila hatua za pamoja na za haraka, mabadiliko ya tabianchi yatazidisha ukosefu wa usawa na kupanua pengo katika maendeleo ya binadamu kulingana na jukwaa jipya lililopewa jina “Human Climate Horizons” lililozinduliwa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP na maabara ya athari za mabadiliko ya tabianchi.