Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Zaidi ya watu milioni 100 kote duniani wamelazimika kufungasha virago na kukimbia makazi yao:UNHCR ripoti
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, lilisema kutokuwa na uhakika wa chakula duniani kote, janga la mabadiliko ya tabianchi, vita nchini Ukraine na dharura nyinginezo kuanzia Afrika hadi Afghanistan ndio sababu kubwa zilizowafanya watu milioni 100 kufungasha virago na kukimbia makwao.
Tusipoilinda bahari tunaathiri kizazi cha sasa na vijavyo: Wananchi wa Vanga Kenya
Ikiwa leo ni siku ya bahari duniani Umoja wa Mataifa imeichagiza dunia kuchukua hatua Madhubuti ili kuhakikishwa inalindwa kwa ajili ya maslhai ya kizazi cha sasa na kijacho kwani bahari sio tu inahakikisha uhakika wa chakula kwa mamilioni ya watu , bali pia ni moja wa muajiri mkubwa na inachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la dunia la kila mwaka.
Mashirika ya Umoja wa Mataifa na wadau wake wametuokoa na ukame Turkana
Eneo la Katilu limenawiri na mimea imechipua. Wakulima wanasubiri kuvuna na kula matunda ya jasho lao.Turkana kusini inakabiliana na ukame kwa kuchimba na kutumia maji ya kisima kwa kilimo na matumizi.
Vita ya Ukraine isipokoma na hatua kuchukuliwa wimbi la watoto wataaga dunia Pembe ya Afrika:UNICEF
Naibu mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, Rania Dagash ameonya leo kwamba "Janga la vifo vya watoto liko karibu kutokea katika Pembe ya Afrika endapo dunia itajikita na vita ya Ukraine na kuyapa kisogo majanga mengine ikiwemo Pembe ya Afrika"
Mabadiliko ya tabianchi yanahatarisha sana afya ya akili na ustawi-WHO
Mabadiliko ya tabianchi yanahatarisha sana afya ya akili na ustawi ndio maana hii leo Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muhtasari wa sera inayo himiza nchi kujumuisha usaidizi wa afya ya akili katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.
Nchi zatakiwa kuimarisha huduma za afya ya akili wakati zikikabiliana na mabadiliko ya tabianchi
Mabadiliko ya tabianchi yanahatarisha sana afya ya akili na ustawi ndio maana hii leo Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO limetoa muhtasari wa sera inayo himiza nchi kujumuisha usaidizi wa afya ya akili katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.
Zaidi ya watu milioni 30 walifungasha virago 2020 kutokana na majanga:UNDRR
Zaidi ya watu milioni 30 walikimbia makazi yao kutokana na majanga mwaka 2020 pekee, na idadi hii huenda ikaongezeka kutokana na kuongezeka kwa hatari na idadi ya matukio makubwa yanayohusiana na hali ya hewa. Jopo katika Kikao cha 7 cha Jukwaa la Kimataifa la Kupunguza Hatari za majanga (GPDR2022), lililosimamiwa na Sarah Charles, Msimamizi Msaidizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani, limeangazia mbinu za kuimarisha utawala ili kupunguza hatari za majanga ya kuhamishwa.
Hatua zichukuliwe sasa kulinda mazingira la sivyo binadamu watageuka kafara: wataalam UN
Miongo mitano baada ya kongamano la kwanza la dunia la kufanya mazingira kuwa suala kuu, wataalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa leo wametoa wito kwa mataifa kuongeza juhudi za kulinda sayari iliyo hatarini kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo huku kukiwa na changamoto ambazo hazijawahi kushuhudiwa za mazingira na nyinginezo.
Baa la njaa lanyemelea Afrika Mashariki ukitabiriwa ukame kwa mwaka wa tano mfululizo:UN
Mashirika sita ya Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa kibinadamu leo wametoa tahadhari ya baa la njaa kunyemelea Afrika Mashariki baada ya miaka minne ya ukame mkali huku ikitabiriwa uhaba wa mvua kwa mwaka mwingine wa tano mfululizo.
Njia 5 za ushirikiano zinazotumiwa na Walinda Amani zinazochangia kuleta amani na maendeleo
Kila siku, walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanafanya kazi ili kuwalinda mamilioni ya watu walio hatarini katika maeneo hatarishi yanayozidi kuwa katika mazingira tete ya kisiasa duniani.