Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Mabadiliko ya Tabianchi
Zaidi ya watu milioni 100 wamelazimika kufungasha virago na kuwa wakimbizi:UN
Katika siku ya wakimbizi duniani Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakimbizi wanawakilisha roho bora zaidi ya kibinadamu.
Hatua za haraka zahitajika huku idadi ya wanaolazimika kuhama makwao ikifikia milioni 110: UNHCR
Vita nchini Ukraine, pamoja na migogoro mingine na machafuko yanayotokana na mabadiliko ya tabianchi, vinamaanisha watu wengi zaidi kuliko wakati mwingine wowote walifurushwa makwao mwaka jana, na hivyo kuongeza udharura wa kuchukua hatua za haraka za Pamoja kupunguza janga hilo la kimataifa limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.
Bahari ni sehemu ya suluhisho la matatizo lukuki katika jamii - FAO
Wakati dunia ikijiandaa kuadhimisha siku ya habari duniani hapo kesho Juni nane shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema ni vyema jamii kuzingatia afya ya baharí kwani umuhimu wake kamwe hauwezi kupuuzwa.
Bahari, ni makazi ya asilimia 80 ya majani ya wanyama, ambayo yanatumika kama chanzo muhimu cha wananchi kujipatia riziki na pia lishe kwa mamilioni ya watu ulimwenguni.
FAO: Bahari ni sehemu ya suluhisho la matatizo lukuki katika jamii
Wakati dunia ikijiandaa kuadhimisha siku ya bahari duniani hapo kesho Juni nane shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO limesema ni vyema jamii kuzingatia afya ya baharí kwani umuhimu wake kamwe hauwezi kupuuzwa.
UNHCR na WFP wazijengea mnepo jamii Tanzania kukabili mabadiliko ya tabianchi
Umoja wa Mataifa umezindua mradi wa miaka mitatu wa kuimarisha mnepo wa jamii dhidi ya mabadiliko ya tabianchi mkoani Kigoma nchini Tanzania ambako mamia kwa maelfu ya wakimbizi wanahifadhiwa.
06 JUNI 2023
Jaridani hii leo tunaangazia ni mada kwa kina na nakupeleka mwambao wa Ziwa Tanganyika nchini Tanzania, hususan mkoani Rukwa ambako huko utasikia harakati za Umoja wa Mataifa za kujumuisha wanawake kwenye uvuvi. Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo za Nishati jadidifu, mabadiliko ya tabianchi na afya. Katika mashinani tunakupeleka nchini Sudan Kusini kusikia ni kwa jinsi gani vijana wanachangia katika mchakato wa utengenezaji wa katiba ukielekea uchaguzi mkuu nchini humo.
Baraza kuu la UNHABITAT laanza Nairobi likijikita na miji endelevu kwa ajili ya kutimiza SDGs
Mkutano wa pili wa Baraza Kuu la shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UNHABITAT umeanza leo mjini Nairobi Kenya ukibeba maudhui “Mustakabali endelevu wa miji kupitia ujumuishwaji na na ufanisi wa ushirikiano wa kimataifa: kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevu wakati wa majanga ya kimataifa.”
Kupunguza taka za plastiki kunahitaji mabadiliko makubwa: UNEP Ripoti
Uchafuzi wa taka za plastiki unaweza kupunguzwa kwa asilimia 80 ifikapo mwaka 2040 ikiwa nchi na makampuni yatafanya mabadiliko ya kina ya sera na masoko kwa kutumia teknolojia zilizopo, kulingana na ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa mazingira UNEP.
Bado Malawi inahitaji msaada wa kibinadamu baada ya kimbunga Freddy
Ikiwa ni mwezi mmoja tangu kimbunga Freddy kupiga wilaya 15 zilizopo kusini mwa nchi ya Malawi na kuathiri maisha ya watu na makazi, jamii hizo bado zinahitaji usaidizi wa kibinadamu ili ziweze kuendelea na maisha wakati huu wakikabiliana na athari za kimbunga hicho ikiwemo mmomonyoko wa udongo.
Licha ya changamoto lukuki watu wa Somalia wanaendelea kuonesha mnepo wa hali ya juu:Guterres
Katika siku ya pili na ya mwisho ya ziara yake nchini Somalia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewapongeza watu wa Somalia akisema licha ya changamoto lukuki zinazowaandama wameendelea kuwa imara na kuonyesha mnepo wa hali ya juu, akiwataka kuendelea kufanya hivyo kwa ajili ya kizazi hiki na kijacho.