Bila amani hakuna haki na bila haki hakuna amani, King tutakuenzi daima:UN
Umoja wa Mataifa umesema mchango na mtazamo wa Martin Luther King Jr aliyekuwa mwanaharakati mkubwa wa haki za binadamu duniani kutakumbukwa na kuenziwa daiama hasa katika zama hizi ambazo dunia imegawika mapende, ukiukwahi wa haki za binadamu unaendelea na chuki na ubaguzi vikimea mizizi.