Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Eneo la Tigray linakabiliwa na changamoto nyingi za kimaendeleao nchini Ethiopia. picha ya maktaba
© UNICEF/Zerihun Sewunet

Tunaendelea kusikitishwa na mauaji na machafuko Tigray:OCHA 

Umoja wa Mataifa umesema unaendelea kusikitishwa na kuendelea kwa taarifa za raia kujeruhiwa na kuuawa kwa raia  wakati wa mapigano yanayoendelea katika maeneo ya vijijini jimboni Tigray nchini Ethiopia na kutiwa hofu kubwa kuhusu janga la maelfu ya watu ambao bado hawajapokea msaada kwenye jimbo hilo kwa zaidi ya miezi miwili na nusu sasa tangu kuzuka kwa machafuko jimboni humo. 

Picha hii kutoka maktaba ikionesha raia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) wakivuka mpaka kwa miguu na kuingia Chad.
© IOM/ Craig Murphy

Heko nchi jirani na CAR kwa kupokea wakimbizi - UNHCR 

Maelfu ya raia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, wakiendelea kumiminika nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Chad, Jamhuri ya Congo na Cameroon kufuatia ghasia mpya zilizoibuka nchini mwao, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limepongeza nchi hizo jiranikwa kufungua mipaka yao na kupokea wakimbizi hao. 

Kituo cha kupima COVID-19 nchini Madagascar
Benki ya Dunia/Henitsoa Rafalia

Maambukizi ya Corona kwa siku Afrika yaongezeka- WHO

Mnyumbuliko mpya wa virusi vinavyosabaisha Corona au COVID-19 barani Afrika umeanza kuenea wakati huu ambapo idadi ya wagonjwa wa virusi wa Corona imefikia milioni 3 na ile ya wagonjwa wapya kila siku ikizidi ile iliyokuwepo wakati wa awamu ya kwanza ya gonjwa hilo.