Nimeshtushwa na serikali ya Ethiopia kutimua maafisa wa UN:Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ameshtushwa sana na kitendo cha serikali ya Ethiopia kuwafurusha maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini humo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema ameshtushwa sana na kitendo cha serikali ya Ethiopia kuwafurusha maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini humo.
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO leo limesema nchi 15 za Afrika ambazo ni karibu theluthi moja ya nchi zote 54 zimefanikiwa kuwachanja kikamilifu asilimia 10 ya watu wake dhidi ya COVID-19.
Wakati janga la tabianchi tayari likiwa limeleta madhara kwa maisha na vipato va watu kote ulimwenguni, vijana watakuwa na nafasi muhimu zaidi katika kusongesha mbele hatua mujarabu, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake kwa vijana wanaoshiriki mkutano tangulizi wa COP-26 huko mjini Milano nchini Italia.
Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya sekta ya bahari , janga la corona au COVID-19 limethibitisha umuhimu wa bahari na kujitolea kwa mamilioni ya mabaharia wanaofanyakazi katika sekta hiyo amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres.
Nchini Tonga, moja ya mataifa ya visiwa vidogo lililoko katika bahari ya Pasifiki, vijana wanafundishwa stadi ya utengenezaji mitumbwi kama njia mojawapo ya kujipatia kipato, kulinda mazingira na kupunguza unene uliopitiliza au utipwatipwa.
Nchini Yemen maisha ya ufukara ni dhahiri miongoni mwa wakimbizi wa ndani ambapo hata kwa wale ambao walibahatika kupata vibarua, ajali kazini imeleta madhila na machungu zaidi na kuzidi kutia mashaka mustakabli wa watoto nchini humo
Suluhu za kitaifa lazima zipatikane kwa watu zaidi ya milioni 55 waliotawanywa kwenye nchi zao kwa mujibu wa ripoti mpya iliyotolewa leo na kuwasilishwa kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na jopo la ngazi ya juu linalojikita na wakimbizi wa ndani.
Kupunguza upotevu na utupaji wa chakula kungechangia uhakika wa chakula, kuimarisha ubora wa chakula na kupunguza uzalishaji wa gesi chafuzi.
Uchumi wa kidijitali unaochochewa na data unazidi kushika kasi lakini wanaonufaka ni wakazi wa nchi tajiri ilhali wale walioko nchi maskini wakiendelea kuwa sehemu ya takwimu lakini si wachuma matunda.
Shirika la Umoja wa mataifa lakuhudumia wakimbizi UNHCR limeitangaza taasisi ya Jeel Albena ya nchini Yemen kuwa mshindi wa mwaka 2021 wa tuzo ya wakimbizi ya Nansen kutokana na kazi nzuri ya kuwasaidia wakimbizi wa ndani nchini humo.