Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa UN António Guterres akihutubia ufunguzi wa jukwaa la kizazi cha usawa hii leo huko Paris nchini Ufaransa
UN

Usawa wa kijinsia waangaziwa zaidi huko Paris Ufaransa

Hii leo huko Paris nchini Ufaransa kumeanza jukwaa la siku tatu la kusaka kusongesha usawa wa kijinsia kwa kujumuisha vijana katika kufanikisha lengo hilo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs ya Umoja wa Mataifa. Mkutano huo unafanyika kwa kuzingatia kuwa miaka 25 baada ya mkutano wa kimataifa wa wanawake huko Beijing nchini China, bado usawa wa jinsia unasalia ndoto kwa maeneo mengi. 

Sauti
3'36"
Shirika la afya duniani WHO linawachagiza vijana barubaru kufanya mazoezi ya viungo na zaidi kwa ajili ya afya na mustakabali wao
Unsplash/Paul Proshin

Hakuna faida ya kungonoka mapema- Kijana balehe

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto -UNICEF nchini Uganda linafadhili mradi wa Mama kwa Mama ambao unajengea uwezo maafisa wa ustawi wa jamii wanaopita kila kaya maskini kusaka  barubaru na vijana balehe waliopata mimba katika umri mdogo na kuwapatia stadi za ufundi ili  hatimaye waweze kujipatia kipato na kubadilisha maisha yao

Sauti
1'52"
Lori lililoratibiwa UNICEF Afrika Kusini na idara za afya za nchi hiyo limekuwa likionyesha video na kutoa matangazo ya watu kuelezea hadithi zao kuhusu COVID-19 kote Afrika Kusini kwa kutumia lugha yao ya mama na kuhamasisha ujumbe wa kupokea chanjo
© UNICEF South Africa

Safari ya lori kuelimisha jamii kuhusu COVID-19 imenifunza mengi:Ntlabati 

Pumla Ntalabati ni mfanyakazi mshauri wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini Afrika Kusini, anasema janga la corona au COVID-19 limemfundisha za mengi, kuanzia amri ya watu kusalia majumbani hadi safari yam ilima na mabonde ya kuelimisha umma katika jimbo la Kwazulu Natal kwa kutumia usafiri wa lori la magurudumu 18.