Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uchumi wa dunia kupungua kwa asilimia 3.1: UN

Benki ya Dunia kutangaza mdororo wa uchumi kwa mwaka huu wa 2022 na kutabiri hali kuwa mbaya zaidi mwakani 2023
United Nations
Benki ya Dunia kutangaza mdororo wa uchumi kwa mwaka huu wa 2022 na kutabiri hali kuwa mbaya zaidi mwakani 2023

Uchumi wa dunia kupungua kwa asilimia 3.1: UN

Ukuaji wa Kiuchumi

Idara ya Umoja wa Mataifa  inayohusika na masuala ya Uchumi na Kijamii imetoa utabiri unao onesha kupungua kwa ukuaji wa uchumi wa dunia hadi asilimia 3.1 kwa mwaka 2022, kutoka asilimia 4.0 iliyo tabiriwa mapema mwezi Januari (2022).

Ripoti ya Hali ya Kiuchumi Duniani na Matarajio yake kwa nusu mwaka  wa 2022 imetolewa leo jijini New York Marekani na imeeleza sababu kubwa za kupungua kwa ukuaji wa uchumi duniani kuwa ni pamoja ya vita inayoendelea nchini Ukraine na janga la coronavirus">COVID-19 ambavyo kwa pamoja zimezidisha kupanda kwa bei za bidhaa  na kuongeza mfumuko wa bei duniani kote.

Mbali na uchumi wa dunia kuathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita nchini Ukraine, kuibuka kwa awamu mbalimbali za mawimbi ya janga la COVID-19 kumefanya hali ya kupata fedha kuwa ngumu zaidi ya ilivyotarajiwa hususan katika nchi zinazoendelea.

Ripoti hiyo imeeleza nchi zinazoendelea ingawa hali ni mbaya lakini pato linatarajiwa kuongezeka kwa asilimia 4.1 kwa mwaka 2022,  hata hivyo kupanda kwa mfumuko wa bei na ukuaji taratibu kwa  polepole kwa nchi za Marekani, China na Umoja wa Ulaya kunatarajiwa kuongeza gharama za kukopa za nchi zinazoendelea na kuzidisha mapengo ya ufadhili.

“Hali ngumu za kifedha za nje zitaathiri vibaya matarajio ya ukuaji wa uchumi hususan kwa nchi zinazotegemea zaidi masoko ya mitaji ya kimataifa, hali hiyo itachangia kuongezeka kwa uhaba wa chakula, hasa barani Afrika.”

Nchi zinapaswa kufanya?

  • Benki kuu katika nchi zinazoendelea zitahitaji kurekebisha viwango vyao vya riba ili kudhibiti shinikizo la mfumuko wa bei, huku zikipunguza athari zake kwa waliokopa na uhimilivu wa deni la taifa.
  • Nchi zinashauriwa kufanya ujuishaji wa mapema inapokuwa inapanga mipango ya masuala ya kifedha ili kudhoofisha hali mbaya ya kiuchumi inayotokana na kuwepo kwa mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za kukopa.
  • Serikali zinahitaji kutoa msaada unaolenga makundi maalum kwenye jamii ili kuzisaidia kupunguza machungu ya kupanga kwa gharama za chakula na mafuta hususan kwa wananchi masikini.

Pia nchi zitahitaji kufanya marekebisho ya kina ya deni na msamaha wa deni kwa nchi maskini, hasa nchi masikini zaidi.

Kusoma ripoti kamili bofya hapa.