Mkataba wa kimataifa wa uhamiaji kupitishwa rasmi Marrakech- UN
Wakuu wa nchi na serikali, mawaziri, viongozi wengine wa ngazi ya juu, asasi za kiraia na wawakilishi toka sekta za umma na binafsi wamekusanyika mjini Marrakech nchini Morocco, kwa ajili ya mkutano wa ngazi ya juu kwa lengo moja tu, kupitisha mkataba wa kimataifa wa uhamiaji.