Kwa miaka 12 ya vita njaa imefurutu ada Syria, hatua zahitajika haraka: WFP
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP amehitimisha ziara yake nchini Syria na kutoa ombi kwa dunia kuwekeza kwa watu wa Syria na jamii zao ili kuwawezesha kujikimu kimaisha na kuacha kutegemea msaada wa chakula.