UNHCR na wadau wasaka dola bilioni 1.3 kwa ajili ya wakimbizi Sudan Kusini
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na washirika wake wanasaka dola bilioni 1.3 mwaka huu ili kushughulikia mahitaji makubwa ya kibinadamu kwa wakimbizi wanaofungasha virago na kukimbia vita vya miaka saba nchini Sudan Kusini.