Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Wanawake wanasubiri msaada wa chakula katika kituo cha usambazaji huko Afgoye, Somalia.
UN Photo/Tobin Jones

Wanawake na Wasichana ndio wahamiaji wengi zaidi katika Mashariki na Pembe ya Afrika - Ripoti ya IOM 

Wanawake na wasichana wameelezwa kuwa ndio idadi kubwa ya wahamiaji Mashariki na Pembe ya Afrika wakiwa ni asilimia 50.4 ya wahamiaji wote ikilinganishwa na wanaume na wavulana, ambao ni asilimia 49.6, jambo ambalo ni la kipekee katika ukanda huo kwa mujibu wa takwimu za kikanda zilizotolewa leo na ripoti ya shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji (IOM) iliyotolewa leo jijini Nairobi, Kenya.