UNMISS imelaani vikali mashambulizi mapya kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani Adidiang Upper Nile
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS, umelaani mashambulizi mapya na ghasia zinazofanywa na watu wenye silaha, zinazolenga wakimbizi wa ndani wanaotafuta hifadhi katika eneo la kisiwa cha Adidiang, kilichoko takriban kilomita 40 kusini mwa mji mkuu wa jimbo la Upper Nile wa Malakal.