Nalaani vikali mashambulizi yanayoendelea dhidi ya raia na wahudumu wa misaada: Nyanti
Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini Sara Beysolow Nyanti,amelaani vikali machafuko yanayoendelea kote nchini ambayo yanaathiri usalama wa raia na wahudumu wa misaada ya kibinadamu , yanatatiza fursa za kufikisha misaada na kuingilia usambazaji wa misaada na huduma kwa watu walio hatarini zaidi.