Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Mfanyakazi wa UNMAS akichunguza mabomu ya kutegwa ardhini, jimbo la Equatoria kati, Sudan Kusini.
© UN Photo/Isaac Billy

UNMAS yaendelea kunusuru maisha ya watu Sudan Kusini kwa kutegua mabomu ya kutegwa ardhini 

Wakati hatua kubwa imepigwa katika kuondoa na kutegua mabomu yote ya kutegwa ardhini na mabaki mengine ya vifaa vya milipuko ya vita nchini Sudan Kusini, baadhi ya jamii za nchi hiyo bado ziko hatarini kutokana na uwepo wa mabomu hayo. Moja ya jamii hizo ni  Gondokoro karibu na mji mkuu Juba, ambako kwa mujibu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa ya huduma za kutegua mabomu ya kutegwa ardhini UNMAS kazi kubwa inaendelea kuyaondoa kabisa mabomu hayo.

Sauti
2'58"