Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Sudan Kusini

Mapigano ya kikabila katika eneo la Jonglei nchini Sudan Kusini yamesababisha utekaji nyara na mauaji. (Maktaba))
UNMISS

UNMISS na wadau wa kimataifa wahofia kuendelea kwa vurugu Greater Pibor na Jonglei

Mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS, mpango wa Muungano wa Afrika Sudan Kusini AUMISS, IGAD, Troika, Muungano wa Ulaya EU na R-JMEC wamesema wana wasiwasi mkubwa kuhusu kuongezeka kwa ghasia, kupoteza maisha na ripoti za madai ya matumizi ya silaha nzito katika Eneo la Utawala la Greater Pibor na vijana wenye silaha kutoka jimbo la Jonglei. 

Mafuriko ya hivi karibuni nchini Sudan Kusini
Picha: UN News

Msaada wa dola milioni 14 kutoka CERF kunufaisha zaidi ya watu 260,000 Sudan Kusini

Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya dharura, Martin Griffiths ametangaza kutoa dola million 14 kutoka mfuko mkuu wa dharura wa Umoja huo, CERF kwa ajili ya kupatia misaada ya kibinadamu wananchi wa Sudan Kusini walioathiriwa na ongezeko la mapigano na mafuriko, kwa kuzingatia kuwa ombi la usaidizi kwa taifa hilo bado uchangiaji wake unasuasua.