Kwa mara ya kwanza hakuna kisa kipya cha Ebola DRC katika siku 7 zilizopita- WHO
Huko nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, hakuna kisa chochote cha Ebola kilichoripotiwa katika siku 7 zilizopita, na hii ni mara ya kwanza tangu mlipuko wa Ebola mwezi Agosti mwaka 2018 nchini humo.