Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

 Kasereka Ngereza, Chifu wa eneo la Oicha kwenye jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, akijadiliana na walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANZBATT-7 waliomtembelea kujadili mbinu za kuimarisha usalama kwenye
TANZBATT 7

Machifu wa Oicha wasema mawasiliano ni muhimu kudhibiti machafuko DRC 

Mawasiliano na elimu kwa vijana na viongozi wa vijiji na mitaa ni jambo muhimu linalopaswa kupewa kipaumbele ili kusaidia vijana kuachana na mawazo potofu na kujiingiza katika magenge ya uhalifu, amesema kiongozi mkuu wa machifu kwenye mji wa Oicha jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC alipokutana na walinda amani wa Umoja wa Mataifa wanaohudumu kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB, cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MONUSCO. Kikosi hicho cha 7 cha Tanzania, TANZBATT kilitembelea eneo hilo ambalo mara kwa mara hukumbwa na machafuko na wamekutana na Kasereka Ngereza, Chifu Mkuu wa eneo la Ochia. 

Sauti
3'7"
Kikundi cha utamaduni cha walinda amani kutoka Tanzania kikifanya onesho kwenye mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

TANZBATT-7 yatumia sanaa kuimarisha amani DRC

Sanaa katika operesheni za ulinzi wa amani zinazofanywa na Umoja wa Mataifa kwenye mataifa mbalimbali ikiwemo Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC imedhihirika  kuwa mbinu muhimu ya kuleta utangamano miongoni mwa wanajamii wa taifa hilo hususan jimboni Kivu Kaskazini kwa kuwa na ujumbe maridhawa wa amani kwa rai na kusahau magumu wanayopitia  kufuatia machafuko yaliyodumu kwa miongo kadhaa.

 

Sauti
3'11"