Nataka na mimi siku moja niitwe “Nellie mmiliki wa duka la kuoka mikate”
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, mradi ulioendeshwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF umewezesha watoto kufungua mradi wao wa kuoka na kupika mikate, mandazi na kalmati na hivyo kuona angalau nuru ya maisha kwenye taifa hilo lililogubikwa na mizozo hususan mashariki mwa nchi.