Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

DR Congo

Mabango ya kampeni za uchaguzi DRC
MONUSCO/M. Asmani

Baraza la Usalama latoa wito kufanyike uchaguzi wa amani DRC

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema uchaguzi wa Desemba 23, mwaka huu 2018 ni ishara ya uhuru wa watu na serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, DRC na ni fursa muhimu katika historia kama uchaguzi wa kwanza unaozingatia demokrasia na ubadilishanaji wa mamlaka kwa amani DRC, na kwamba ni fursa ya kujenga msingi wa amani na kuweka mazingira kwa ajili ya maendeleo ya nchi hiyo.

Msafara wa wahamiaji wa Amerika ya kati ukipita Chiapas Mexico (2018)
IOM / Rafael Rodríguez

Uhamiaji uwe wa utu kwa kila mtu- IOM

Katika kuadhimisha siku ya uhamiaji duniani hii leo, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM, António Vitorino ametaka hatua zaidi na za dharura zichukuliwe ili kulinda kundi hilo ambalo kila uchwao linakumbwa na madhila kote ulimwenguni.

Wakimbizi kutoka Iran, Venezuela, Syria, Afghanistan na Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR
UNHCR/UNICEF

Mkataba wa kimataifa wa wakimbizi kupitishwa leo

Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Baraza Kuu la chombo hicho litapitisha mkataba wa kimataifa wa wakimbizi na hivyo kusaidia kwa kiasi kikubwa wale wanaokimbia makwao na nchi zinazowahifadhi, ambazo mara nyingi ni zile maskini zaidi duniani. Siraj Kalyango na maelezo zaidi.