Sasa mkataba wa Marrakech ni rasmi, Baraza Kuu la UN laupitisha
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limepitisha kwa kishindo mkataba wa kimataifa wa uhamiaji salama, wenye mpangilio na unaofuata kanuni za kawaida.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limepitisha kwa kishindo mkataba wa kimataifa wa uhamiaji salama, wenye mpangilio na unaofuata kanuni za kawaida.
Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa leo inaonyesha kuendelea kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, ikiwemo mauaji ya mamia ya watu, visa vya utesaji na ukatili wa kingono dhidi ya raia katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema uchaguzi wa Desemba 23, mwaka huu 2018 ni ishara ya uhuru wa watu na serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo, DRC na ni fursa muhimu katika historia kama uchaguzi wa kwanza unaozingatia demokrasia na ubadilishanaji wa mamlaka kwa amani DRC, na kwamba ni fursa ya kujenga msingi wa amani na kuweka mazingira kwa ajili ya maendeleo ya nchi hiyo.
Wakati machafuko yakiendelea kusambaratisha familia na kuwalazimisha kufungasha virago nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC maelfu ya wakimbizi wa ndani wanatafuta faraja kwa kusaidiana kupitia ushirika ulioanzishwa kwa minajili ya kuchagiza ulinzi wa haki za binadamu na kusaka suluhu ya changamoto zinazowakabili
Katika kuadhimisha siku ya uhamiaji duniani hii leo, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM, António Vitorino ametaka hatua zaidi na za dharura zichukuliwe ili kulinda kundi hilo ambalo kila uchwao linakumbwa na madhila kote ulimwenguni.
Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Baraza Kuu la chombo hicho litapitisha mkataba wa kimataifa wa wakimbizi na hivyo kusaidia kwa kiasi kikubwa wale wanaokimbia makwao na nchi zinazowahifadhi, ambazo mara nyingi ni zile maskini zaidi duniani. Siraj Kalyango na maelezo zaidi.
Mkataba wa kimataifa wa wakimbizi: Tofauti ni ipi na mkataba wa wahamiaji na ni kwa vipi utasaidia watu waliolazimika kukimbia makwao?
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, lina wasiwasi na idadi kubwa ya watu ambao wameachwa bila makazi kutokana na mapigano yanayoendelea nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, msemaji wa shirika hilo Charlie Yaxley amenukuliwa leo mjini Geneva Uswisi.
Ikiwa zimebakia siku 9 kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Kamishna Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet ameelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya ghasia zilizoripotiwa katika majimbo matatu nchinu humo wiki hii wakati wa kampeni za uchaguzi.
Ikiwa mwezi huu ni umetimu mwaka mmoja tangu walinda amani 15 wa Tanzania wauawe huko Semuliki jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC, Umoja wa Mataifa umesema katu hautosahau mchango wao na utaendelea kuenzi kazi yao.