Mashambulizi dhidi ya raia yaongezeka Beni: UNHCR
Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR limesema lina wasiwasi kuhusu usalama wa maelfu ya raia katika eneo la Kaskazini Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, DRC ambako ghasia za makundi yenye silaha zimeongezeka na za hivi karibuni zimesababisha vifo vya watu zaidi ya 20. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi.