Kesi ya mbabe wa kivita Ntabo Ntaberi Cheka imeanza kuunguruma DRC:
Kesi ya mbabe wa zamani wa kivita kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Ntabo Ntaberi Cheka imeanza kusikilizwa mjini Goma jimbo la Kivu ya Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Kesi ya mbabe wa zamani wa kivita kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Ntabo Ntaberi Cheka imeanza kusikilizwa mjini Goma jimbo la Kivu ya Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo.
Nchini Tanzania hii leo walinda amani watatu wa taifa hilo waliouawa katika matukio tofauti ya mapigano huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wameagwa rasmi katika tukio lililoongozwa na Waziri wa Ulinzi Dkt. Hussein Mwinyi.
Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamesema wanaamini kuwa uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC tarehe 23 mwezi ujao wa Disemba ni fursa ya kihistoria kwa uchaguzi wa kidemokrasia na wa amani kwenye nchi hiyo ya Maziwa Makuu barani Afrika.
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa María Fernanda Espinosa, amesema anaelewa fika uamuzi wa baadhi ya mataifa wa kutokuwa tayari kutia saini makubaliano mapya kuhusu uhamiaji baadaye mwaka huu.
Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP limesema linaendelea na mgao wa chakula na usambazaji wa vifaa kwenye maeneo yaliyokumbwa na mlipuko wa Ebola huko Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Shirika la afya duniani WHO limesema kazi za kupambana na mlipuko wa ugonjwa Ebola Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo DRC baado zinaendelea licha mashambulio yaliyofanywa Ijumaa katika mji Beni nchini humo.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, huduma ya utoaji wa matibabu bure kwenye maeneo yaliyokumbwa na mlipuko wa Ebola, haujawa na matokeo chanya kama ilivyotarajiwa.
Walinda amani 7 wa Umoja wa Mataifa wameuawa huko Beni, jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema sasa kuna matumaini makubwa ya kupitishwa kwa mkataba wa kimataifa kuhusu wakimbiz na wahamiaji, GCM mwezi ujao.
Hatua mpya za kukabiliana na changamoto za vita dhidi ya mlipuko wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC zinazaa matunda ingawa mlipuko huo bado unasalia kuwa hatari na usiotabirika.