Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
MJADALA MKUU WA UNGA74

Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu  Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.

Visiwa vya Tuvalu viko katika hatari ya kuongezeka kwa kina cha maji ya bahari kutokana na mabadiliko ya tabia nchi.
UNDP Tuvalu/Aurélia Rusek

Nchi 38 zinazoendelea za visiwa vidogo, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi

Nchi 38 zilizotambuliwa na Umoja wa Mataifa kama nchi zinazoendelea za visiwa vidogo, au SIDS, ni kati ya nchi zilizo hatarini zaidi ulimwenguni. Nchi hizi ambazo ziko kwenye eneo la Karibea, bahari ya Pasifiki, ya Atlantiki, ya Hindi na Bahari ya Uchina ya Kusini zinaathirika na hali inayozidi ya mabadiliko ya tabianchi ulimwenguni ambayo haitabiriki. Pamoja na changamoto za mazingira, SIDS inakabiliwa na seti ya kipekee ya masuala yanayohusiana na udogo na umbali.