Ukinzani wa sheria ni kikwazo cha umiliki ardhi miongoni mwa wanawake Tanzania- LANDESA
Mkutano wa 62 wa hali ya wanawake duniani, CSW62 ukiendelea kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, hoja ya umiliki ardhi imetamalaki miongoni mwa washiriki. Wawakilishi wa wanawake na wasichana wa vijijini pamoja na wanawake wenyewe wanabadilishana uzoefu juu ya kile cha kufanya ili kuhakikisha kuwa umiliki wa ardhi unafanyika bila kujali jinsia ya mtu.