Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Kutoa ni moyo wala si utajiri

Kutana na mama Shamsa Abdilahi, yeyé na mumewe walikuwa wakimbizi kutoka Somalia ambao wameishi Uingereza kwa miaka kadhaa. Ametambua umuhimu wa kusaidia alipokuwa na mahitaji, na akaahidi kurejea nyumbani mambo yatakapokaa sawa ili kurejesha hisani.

Audio Duration
4'21"
UN News/Patrick Newman

Nachukizwa sana na wanaoona wenye shida ni ombaomba- Brenda

Kwa siku nne kuanzia tarehe 8 Februari 2018 vijana kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa walikutana jijini New York, Marekani kwa ajili ya mjadala wa mustakhbali wa dunia. Mjadala huo wa vijana umefanyika kwa kuzingatia mfumo wa Umoja wa Mataifa, ikiwa ni mojawapo ya njia ya kuwandaa vijana kubeba jukumu la kusongesha maendeleo kwenye nchi zao na dunia kwa ujumla. Miongoni mwao ni Brenda Kimwatan, mwanafunzi kutoka Kenya ambaye anasoma Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini.

Sauti
4'10"

Mkimbizi anatafuta maisha - JJ Bola

Umoja wa Mataifa unaendelea kusisitiza kuwa mtazamo potofu kuhusu uhamiaji na wahamiaji umeendelea kukwamisha matumizi bora ya dhana hiyo kote ulimwenguni. Umoja huo unahimiza serikali zote kuenzi mbinu tofouti za kufanya uhamiaji uwe na manufaa kwa wote, maana wakimbizi wanaweza kuchangia katika uchumi ya nchi wanamoishi. Licha ya wito huo bado wakimbizi wengi bado wanapitia machungu wanapokuwa ukimbizini, kitu ambacho kinasababisha wengi kuwaza walikotoka na machungu walioyapitia.

Sauti
3'55"

Viwanda vidogovidogo vyalaumiwa kuchafua vyanzo vya maji

Maji safi na salama ni uhai wa viumbe vyote ulimwenguni ikijumuisha binadamu, wanyama na mimea. Lengo namba 6 la  malengo ya maendeleo  endelevu, SGD linazungumzia maji safi na salama kwa kila mtu ifikapo  ya mwaka 2030.

Katika migogoro ya kimazingira, viwanda vidogo na vikubwa vimekuwa vikilalamikiwa kuharibu mazingira kwa kujenga mifereji inayopeleka maji taka katika vyanzo vya maji au mito.

Sauti
3'55"

Ni wakati wa vijana kuamka na kupiga kelele

Ripoti ya hivi karibuni ya shirika la kazi duniani, ILO  inaonyesha kuwa soko la ajira kwa vijana katika nchi zinazoendelea hususan katika bara la Afrika, Amerika kusini na Asia kusini linazidi kusuasua kutokana na ukuaji mdogo wa uchumi katika nchi hizo.

Umoja wa mataifa katika ajenda 2030 ya maendeleo endelevu au SDGs , inazihimiza serikali,  mashirika na asasi za kiraia kuwekeza katika taaluma au miradi itakayowawezesha vijana kujikwamuwa na tatizo la ajira ifikapo mwaka2030.

Sauti
2'54"
PICHA:IOM/Muse Mohammed

Makala ya Assumpta Massoi kuhusu bendi ya wakimbizi huko Brazil.

Nchini Brazil wakimbizi kutoka maeneo 10 tofauti duniani kuanzia Afrika hadi Asia na Mashariki ya Kati wameungana ili kutumia lugha moja inayofahamika zaidi duniani kusuuza siyo tu roho zao bali jamii  inayowazunguza. Wanamuziki hawa wanatumia lugha ya muziki wakisema kuwa ndicho kinawapeleka walikotoka kwa sababu mbalimbali ikiwemo vitisho, mauaji au ghasia. Je wanafanya nini huko Brazili? Ungana basi na Assumpta Massoi katika makala hii iliyowezekana kufuatia usaidizi wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR.

Sauti
4'3"

Paschal Masalu wa ElimikaWikiendi ahojiwa na Habari za UN

Vijana wana mchango mkubwa katika kusongesha ajenda ya mwaka 2030 ya maendeleo endelevu au SDGs . Hayo yamesisitizwa katika jukwaa la vijana la Umoja wa Mataifa 2018 lililokunja jamvi hii leo kwenye makao makuu ya Umoja huo New York Marekani. Vijana 700 kutoka nchi mbalimbali wamejadili jinsi gani washirikishwe na mchango wao katika kufanikisha azma hiyo ya Dunia. Miongoni mwa waliohudhuria ni kijana Paschal Masalu kutoka nchini Tanzania ambaye ni afisa mtendaji wa jukwaa la Elimikawikiendi nchini humo.

Sauti
3'43"

Ukatili dhidi ya wakawake marufuku Burundi: Seruka

Ukatili wa kijinsia ni changamoto kubwa nchini Burundi huku Zaidi ya asilimia 90 ya wanaotendewa ukatili huo wakiwa ni wanawake na watoto. Sasa shirika lisilo la kiserikali la SERUKA limeamua kushikia bango dhuluma hiyo kwa kuendesha kampeni katika maeneo mbalimbali nchini humo kupinga na kuelimisha jamii kuachana na ukatili dhidi ya wanawake. Mwandishi wetu wa maziwa makuu Ramadhan Kibuga alitembelea moja ya kampeni za shirika hilo kwenye uwanja wa Parke mjini Bujumbura uangana naye kwenye Makala hii.

Ngoma ya vinyago yainyanyua Cote d'Ivoire

Utamaduni ni kielelezo cha utashi wa kila jamii ambapo kupitia utamaduni huo jamii hujielezea ilivyo na kujitambulisha pia kwa jamii zingine. Nchini Cote d' Ivoire katika jamii ya Guro, ngoma yao inayotumia vinyago imekuwa na manufaa kwa jamii na nchi nzima hadi kutambuliwa na Umoja wa Mataifa. Je ni ngoma ya aina gani? Ungana basi na Assumpta Massoi kwenye makala hii.