Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

World Bank/Arne Hoel

Kijana si lazima aajiriwe kupitia mafunzo anaweza kujiajiri:Nyoni TYC

Changamoto kubwa inayowakabili vijana kote duniani ni ajira hata kama wana elimu ya kutosha kuajiriwa. Kwa kutambua changamoto hiyo taasisi ya vijana nchini Tanzania (TYC) imechukua hatua ya kuhakikisha vijana wanaelemishwa uwezo walio nao katika ujasiriamali na kuweza kusaidia kuziba pengo la ajira hasa katika utimizaji wa lengo namba 8 la maendeleo endelevu au SDGs linalozungumzia ajira zenye staha.

Sauti
4'10"
UN News/Assumpta Massoi

Linalowezekana kufanyika kujipatia kipato fanya usibweteke:Wanawake Dodoma

Kazi za kuajiriwa ofisini imekuwa mtihani mkubwa kwa wanawake wengi hususan barani Afrika, na ujasiriamali umekuwa ndio kimbilio na mkombozi kwa waliosoma na hata wasio na elimu kwani kinachohitajika ni juhudi na maafifa. Hii ni moja ya kauli zilizotolewa na wanawake wajasiriamali kutoka mkoani Dodoma nchini Tanzania wanaojiuhusisha na kazi mbalimbali ikiwemo za udereva wa pikipiki ya magudurudumu matatu ali maarufu kama Bajaji.

Sauti
3'24"
UN-Habitat/Nathan Kihara

Wanaoishi katika makazi duni wanahitaji mnepo dhidi ya mabadiliko ya tabianchi:UN-HABITAT

Mamilioni ya watu wanaoishi katika mitaa ya mabanda au makazi dunia kote duniani wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo miundombinu mibovu, ukosefu wa maji safi na salama n ahata hali mbaya ya Maisha lakini kubwa zaidi kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la makazi duniani UN-HABITAT ni kutokuwa na mnepo wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi. Shirika hilo linasema vimbunga au mafuriko yanapozuka wao huwa wa kwanza kuathirika na hasara yake ni kubwa Zaidi kuliko wengine.

Sauti
4'8"
UNFPA

Wakunga wapaza sauti kuhusu changamoto kazini

Wakunga na wauguzi huwa msitari wa mbele kwenye shughuli nyingi za kitabibu na hivyo huchangia sehemu muhimu ya huduma za afya.

Lakini licha ya hayo mara nyingi hulaumiwa na umma wakidai wanazembea kuwahudumia sanjari na matarajio.

Kazi zote kawaida huwa na mapungufu ambayo ni vyema yashughulikiwe kwa njia za amani kwa kujadiliana badala ya kulaumiana, ndivyo wanavyosema wakunga nchini Uganda kwenye mkutano wa wadau uliokuwa motomoto ukisaka njia za kuboresha huduma za afya.

Sauti
3'42"
Unsplash/Markus Spiske

Wahenga walinena penye nia pana njia usemi ambao msichana Regina Honu ameutimiza

Kutana na msichana Regina Honu kutoka Ghana ambaye usemi wa wahenga penye nia pana njia haukumpa kisigo. Alipokuwa na umri wa miaka 12 aliifahamu kompyuta kwa mara ya kwanza na akaipenda sana hasa kupitia mchezo unaoitwa Pacman na akataka kuanzisha wa kwake ,na ndoto yake ya kuwa msichana wa teknolojia ikatimia kwani  leo hii Regina ni mwanzilishi wa shirika lisilo la kiserikali liitwalo “Tech Needs girls” au teknolojia inahitaji wasichana.

Sauti
2'42"
© UNICEF/Karel Prinsloo

Mabaya mengi yanayosemwa kuhusu wakunga/wauguzi sio- Bi. Mafuru

Wakati dunia ikiwa katika muongo wa mwisho kuelekea kutimiza malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa yenye ukomo wake mwaka 2030, kuna mwamko mpya kwa nchi wanachama kutimiza malengo hayo ikiwemo lengo namba Tatu la afya kwa wote. 

Katika kufanikisha lengo hilo, wakunga na wauguzi wana mchango mkubwa kwani afya ya uzazi ni moja ya sekta ambazo bado inakabiliwa na changamoto ikiwemo nguvu kazi.  

Sauti
3'56"
© UN-Habitat/Kirsten Milhahn

Mradi wa Benki ya Dunia waleta nuru kwa wakazi wa mtaa duni Kenya

Nchini Kenya ukuaji wa miji umekuwa na athari kubwa katika matumizi ya maji na usimamizi wa majitaka katika miji mingi, ambayo tayari inakabiliwa na ongezeko la mahitaji ya maji na huduma ya kujisafi, kwa mfano uchafuzi na matumizi kupitiliza.

Kupitia msaada wa Benki ya Dunia, takriban watu 85,000 katika makazi ya mabanda kwenye mji mkuu wa Kenya, Nairobi, sasa wanaweza kupata huduma ya maji na mtandao wa majitaka. Katika Makala hii, Assumpta Massoi amefuatilia mradi ambao umebadilisha maisha ya wakazi katika eneo hilo, ungana naye.

Sauti
3'30"
© UNICEF/Karin Schermbrucke

Juhudi za wakunga na wauguzi kuhudumia jamii wilaya ya Pangani, Tanzania

Mwaka wa 2020 ni mwaka wa kutambua mchango wa wauguzi na wakunga katika kufanikisha afya kwa wote. Nchi mbalimbali kwa kutambua mchango wa watu hawa, zimechukua hatua kuwawezesha licha ya kwamba bado idadi ya wauguzi kwa wagonjwa katika nchi nyingi haijafikia viwango vinavyohitajika.

Tanzania ni moja ya nchi ambazo zinaendelea kuweka msistizo katika kuimarisha idadi ya wauguzi kwenye hospitali. Katika Makala hii, Saa Zumo wa radio washirika amevinjari hospitali ya Pangani na haya ni mahojiano yake na mgeni wa leo anaanza kwa kujitambulisha

Sauti
4'59"
© UNICEF

Ukunga na uuguzi ni wito- Bwana Abdalla

Wakati dunia ikiadhimisha mwaka wa wakunga na wauguzi kutokana na mchango wa wahudumu  hao wa afya, shirika la afya ulimwenguni, WHO limesema sekta ya afya inahitaji huduma zaidi ya kundi hilo kwa kuwa wana mchango mkubwa katika kufanikisha huduma za afya na hivyo kufikia malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, hususan lile namba 4 la afya na ustawi.

Sauti
4'3"
UNFPA Mozambique

Nilivutiwa kuwa muuguzi kwa sababu mama yangu alikuwa muuguzi-Jackline Ayuma

Wakati dunia ikiadhimisha mwaka wa wakunga na wauguzi, shirika la afya ulimwenguni limesema nguvu kazi thabiti ya kundi hilo ni muhimu katika kufikia afya kwa wote.

Hatahivyo, WHO imesema mara nyingi wauguzi na wakunga hawathaminiwi na hushindwa kufikia uwezo wao kamili. Mwaka 2020 tunalenga kuhakikisha kwamba wauguzi na wakunga wanafanya kazi katika mazingira ambayo ni salama, wanakoheshimiwa na wafanyakazi wenzao na wanajamii na kwmaba wanafikia huduma ya afya na wanakofanyia kazi wanajumuishwa na wataalam tofauti wa kiafya.

Sauti
2'41"