Kijana si lazima aajiriwe kupitia mafunzo anaweza kujiajiri:Nyoni TYC
Changamoto kubwa inayowakabili vijana kote duniani ni ajira hata kama wana elimu ya kutosha kuajiriwa. Kwa kutambua changamoto hiyo taasisi ya vijana nchini Tanzania (TYC) imechukua hatua ya kuhakikisha vijana wanaelemishwa uwezo walio nao katika ujasiriamali na kuweza kusaidia kuziba pengo la ajira hasa katika utimizaji wa lengo namba 8 la maendeleo endelevu au SDGs linalozungumzia ajira zenye staha.