Wanawake waimarisha ushiriki kwenye siasa za Uganda
Kufuatia juhudi za shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake, UN Women za kuwezesha wanawake, kupitia wadau mbalimbali duniani kote, kumekuwa na hatua chanya katika nchi kadhaa zikiwemo zile za Afrika Mashariki.
Kwa sasa ni bayana kwamba wanawake wanajitokeza kugombea nafasi mbalimbali za kisiasa na mara nyingine kuwashinda wanaume hali hiyo ikiwa ni tofauti na zamani ambapo ulikuwa ni mwiko kwa mwanamke kusimama mbele hadharani na kuongea.