Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN Kenya/Newton Kanhema

COVID-19 imenirudisha nyumbani kijijini-Waweru

Tangu lizuke janga la corona duniani athari nyingi za karibu kila sekta zimeshuhudiwa. Vijana ambao idadi yao ndiyo kubwa kwa karibu kila nchini duniani nao wameathirika pakubwa. Wengi walilazimika kusitisha masomo kufuatia kufungwa shule na taasisi za elimu, wengine wakapoteza ajira na kubaki katika hali ya sintofahamu kuhusu hatma ya maisha yao. Kijana Joseph Waweru alipoteza kibarua chake mjini Nairobi na pia mipango yake ya masomo katika chuo kikuu ikakwama ndipo akaamua kuhamia kwao alikozaliwa huko Kitale, magharibi mwa Kenya.

Sauti
3'35"
© ITU/M. Jacobson – Gonzalez

Apps and Girls, taasisi iliyodhamiria kuwainua wasichana katika TEHAMA nchini Tanzania

Ni ukweli ulio wazi kwamba duniani kote bado kuna pengo kubwa la wasichana katika teknolojia ya mawasiliano yaani TEHAMA ingawa juhudi za hivi karibuni, kimataifa na kitaifa zinaonesha kuanza kuzaa matunda kwani wasichana wanazidi kushawishika kuingia katika masomo yanayohusisha TEHAMA. Mafaniko ya juu ni vigumu kuyafikia ikiwa jamii kwa ujumla kuanzia mtu mmojammoja hatahusika katika kuweka mazingira kwa wasichana kupata ujuzi wa teknolojia ya mawasiliano. 

Sauti
3'46"
UNICEF/Tremeau

Msitu wa Bugoma ni uhai kwa maisha yetu-Uganda

Misitu ya asili kote duniani, kwa miaka mingi imekuwa sehemu muhimu ya maisha ya binadamu. Mathalani nchini Uganda, msitu wa Bugoma si tu unatunza historia ya asili ya watu wa eneo hilo, bali pia, wakazi wa eneo hilo wanasema vyanzo vingi vya maji ya mito ya eneo hilo ni katika mstu huo ambao pia unawapa dawa za asili za mitishamba zinazotumika katika tiba ya asili ya kiafrika. Katika makala ifuatayo, John Kibego, mwandishi wetu wa Uganda anapeperusha hewani maoni ya  wenyeji wa msitu wa Bugoma kuhusu tishio la kuchafuliwa kwa kiasi kukubwa cha msitu huo wa akiba.

Sauti
3'4"
© UNHCR/Rocco Nuri

Watoto wakimbizi wahusishwa katika kupambana na COVID-19 Uganda

Mlipuko wa COVID-19 duniani umetia mashakani karibu malengo yote ya Maendeleo endelevu au SDGs baada ya kukwamisha elimu, usafiri na uchumi miongoni mwa mengine. Hali imekuwa mbaya zaidi miongoni mwa wakimbizi kutokana na changamoto za uhaba wa rasilimali ambazo kawaida huwakumba hasa idadi yao inapoongezeka  bila kutarajiwa. Hata hivyo, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR na wadau wake nchini Uganda wameanzisha ushirikishwaji wa watoto wakimbizi katika juhudi za kupambana na COVID-19 wakati huu ambapo takribani wakimbizi mia moja wameambukizwa.&nbs

Sauti
3'24"
UN/Ahimidiwe Olotu

Ikiwa una ndoto lakini unahisi unaelekea kukata tamaa kutokana na vikwazo, sikiliza hii.

Katika maisha yake yote hadi sasa, kijana Narsent Charles Meena, ameishi na ndoto yake ya kusomea urubani ili siku moja aweze kuendesha ndege. Ndoto yake hiyo tayari imemfikisha katika kufanya kazi katika viwanja vya ndege na hata kufanya kazi katika ndege. Jambo moja ambalo hata hivyo hajalifikia ni kuendesha ndege. Je, karanga za shilingi 500 anazoziuza zitamwezesha kupata shilingi milioni 150 za Tanzania sawa na takribani dola elfu 65 ili aweze kusomea urubani? Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha habari za Umoja wa Mataifa amemhoji kijana huyu.

 

Sauti
3'29"
UNMISS\Nektarios Markogiannis

Mitandao ya intaneti ina taarifa nyingi, ukichagua zinazofaa, unafanikiwa-Gladys Njoki Maina

Wakati Gladys Njoki Maina alipomaliza Chuo Kikuu mwaka 2017 alipata changato za kupata  kazi jijini Nairobi lakini hakufa moyo. Kutokana na kwamba nywele zake zilimpa changamoto  alifikiria na kubuni njia za kuzirembesha zaidi ndipo kwa kutumia ujuzi aliojisomea katika mitandao ya intaneti akavumbua mafuta kwa jina GeenyLove. Mafuta hayo yamepata na umaarufu miongoni mwa akina dada ndani na  nje ya Kenya kwa kusaidia kurembesha nywele za kiafrika. Gladys sasa ana kampuni ya kutengeneza mafuta ya nywele na amezungumza na Jason Nyakundi kuhusu safari yake.

Sauti
3'35"
UNICEF/Adriana Zehbrauskas

Zaidi ya mara moja, nilijaribu kujiua.

Tukielekea siku ya kimataifa ya kupinga na kuzuia kujiua ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 10 mwezi huu wa Septemba, ikiwa kama njia ya kuchukua hatua za dunia nzima kuzuia watu kujiua huku shughuli tofauti zikifanyika kote dunia tangu mwaka 2003, Mwandishi wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na vijana ambao wakati mmoja walijaribu kujitoa uhai kwa sababu moja au nyingine. Ili kufahamu kilichosababisha hadi wao kuwaza hivyo, walinusurika kwa njia gani, na sasa maisha yao yamebadilika kwa njia gani, kwako Jason Nyakundi.

Sauti
8'7"