Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maziwa ya ng'ombe yana protini isiyoweza kumeng'enywa kwenye tumbo la mtoto mwenye umri wa chini ya miezi 6 - Mtaalamu

Maziwa ya ng'ombe yana protini isiyoweza kumeng'enywa kwenye tumbo la mtoto mwenye umri wa chini ya miezi 6 - Mtaalamu

Pakua

Ni mwaka mmoja tangu mradi wa mafunzo kuhusu lishe endelevu ulipoanzishwa mkoani Morogoro kwa ufadhili wa shirika la Save the Children na shirika la Marekani la msaada wa kimataifa USAID. Sehemu ya mradi huo ni kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa mtoto kunyonya maziwa halisi ya mama angalau kwa miezi sita ya kwanza. Je, wanuafaika wa mradi huo wanasemaje? Wameelimika kwa kiasi gani tangu mradi huo kuanzishwa mwezi Agosti mwaka jana 2019? John Kabambala wa redio washirika Kids Time FM amezungumza nao na kuandaa makala hii. 

Audio Credit
Loise Wairimu\John Kabambala
Audio Duration
3'25"
Photo Credit
© UNICEF/Zahara Abdul