Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kuna pengo kubwa kati ya wanaume na wanawake kwenye tasnia ya upigaji picha Tanzania -Nsamila

Kuna pengo kubwa kati ya wanaume na wanawake kwenye tasnia ya upigaji picha Tanzania -Nsamila

Pakua

Nchini Tanzania, mpiga picha maarufu, Imani Nsamila kwa kushirikiana na shirika la Ladies Joint Forum na Kikoi innovative media, kwa siku tano wamewapa mafunzo ya upigaji picha wasichana 28 ikiwa ni moja ya harakati za kuyafikia malengo Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs, kama vile lengo namba 5 linalolenga ulimwengu kuwa na usawa wa kijinsia kufikia mwaka 2030. Ahimidiwe Olotu wa Kituo cha habari cha  Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam amemhoji Imani Nsamila ambaye anaanza kwa kueleza alisukumwa na nini kuanza na kundi hili? 

 

Audio Credit
Loise Wairimu\Ahimidiwe Olotu
Audio Duration
3'24"
Photo Credit
UN/Imani Nsamila