Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

© UNICEF/UNI342042/

Janga la COVID-19 halikumzuia mzazi Ghana kuhakikisha watoto wanaendelea kujifunza

Nchini Ghana, janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 lililoibuka mwezi Machi mwaka jana wa 2020 lilitikisa shughuli za kisiasa, kiuchumi na kijamii. Mathalani shule zilifungwa na hivyo kutikisa pia ari ya wazazi waliokuwa wakijitolea kufundisha hasa katika shule zilizoko vijijini. Mwelekeo wa kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs hususan namba 4 kuhusu elimu bora ulikuwa mashakani. Wazazi walishajitolea kusaidia maeneo ya vijijini lakini kufungwa kwa shule kukaleta hofu.

Sauti
3'31"
UN Women/Müslüm Bayburs

Hellen Obiri, mwanajeshi kutoka jeshi la anga la Kenya anayetamba duniani kwa mbio 

Umoja wa Mataifa unasisitiza kuwa michezo ina uwezo wa kubadili dunia, ni haki ya msingi, nyenzo muhimu ya kuimarisha mshikamano wa kijamii na kuchagiza malengo ya maendeleo endelevu, amani, mshikamano na kuheshimiana na ndio maana katika makala ya leo tunamwangazia Hellen Obiri mwanariadha kutoka jeshi la anga la Kenya bingwa wa dunia mbio za mita 5,000.  Obiri alizaliwa huko Kisii magharibi mwa Kenya lakini kwa jitihada zake amefanikiwa kufikia kiwango cha mwanariadha wa kimataifa anayesifika.

Sauti
3'44"
© FAO/IFAD/WFP/Petterik Wiggers

Ili kutokomeza njaa Tanzania tunapambana na mizizi ya tatizo hilo:WFP 

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP limesema njaa ni tatizo mtambuka ambalo linachangia nchi nyingi kushindwa kufikia malengo ya maendeleo endelevu SDGs. Na ili kutimiza malengo hayo nchini Tanzania WFP imeweka mkakati wa miaka mitano kushughulikias maeneo matano ambayo ni mizizi ya tatizo hilo ili kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2030 ukomo wa utekelezaji wa SDGs lengo namba 2 la kutokomeza njaa linatimia pamoja na malengo mengine. Je ni maeneo gani hayo? Tuungane na Ahimidiwe Olotu wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam Tanzania. 

Sauti
4'35"
UN Women /Aidah Nanyonjo

Wasichana wapata stadi za kuwasaidia kustawi licha ya  COVID-19 na mafuriko nchini Uganda

Mafuriko ya mara kwa mara makazi hasa katika maeneo ya ziwa Albert nchini Uganda sambamba na athari za COVID-19 yameathiri ustawi wa watu katika matabaka mbalimbali. Vijana hasa wa kike wanaripotiwa kuingia katika hatari za kubakwa, na kutumbukia kwenye ndoa za utotoni na madhara yake. Kikundi cha Kaiso Women’s Group kwenye Ziwa Alebrt wilayani Hoima wanajitahidi kupambana na hali hiyo kwa kuwsafunza baadhi ya wasichana pamoja na wanawake ufundi cherehani na utengenezaji wa sabuni miongoni mwa mengine ambayo tayari vimeleta nuru.

Sauti
3'38"
UN News/ John Kibego

Wasichana wapata stadi za kuwasaidia kustawi licha ya  COVID-19 na mafuriko nchini Uganda

Mafuriko yanayozidi kukosesha watu wengi makazi hasa katika maeneo ya ziwa Albert nchini Uganda sambamba na athari za COVID-19 yameathiri ustawi wa watu katika matabaka mbalimbali.Vijana hasa wa kike wanaripotiwa kuingia katika hatari za kubakwa, na kutumbukia kwenye ndoa za utotoni na madhara yake. Kikundi cha Kaiso Women’s Group kwenye Ziwa Alebrt wilayani Hoima wanajitahidi kupambana na hali hiyo kwa kuwsafunza baadhi ya wasichana pamoja na wanawake ufundi cherehani na utengenezaji wa sabuni miongoni mwa mengine ambayo tayari vimeleta nuru.

Sauti
3'38"
UNICEF/Jimmy Adriko

UNHCR yaeleza matukio ya wakimbizi na kuwatia moyo mwakani, Uganda

Mwaka 2020 umekuwa wenye changamoto nyingi zilizoathiri watu wa tabaka mbalimbali ingawa kwa viwango tofauti.

Janga la COVID-19, mafuriko katika maeneo mbalimbali na halikadhalika janga la uvamizi wa nzige katika eneo la Pembe mwa Afrika na Afrika Mashariki yalivuruga maisha kiuchumi na kijamii.

Haya yote yamekuwa na madhara hasa kwa jamii zilizohatarini wakiwemo wakimbizi.

Sauti
3'47"
UNICEF/Jimmy Adriko

Pamoja na changamoto ya COVID-19, kijana mkimbizi Uganda ajivunia mafaniko.

Licha ya mlipuko wa COVID-19 nchini Uganda kuenea hadi katika makambi ya wakimbizi ikiwemo Kyangwali na kuathiri uchumi na maisha kijamii, baadhi ya wakimbizi wamepata mafanikio na kuwa matumaini na mwaka ujao wa 2021.

Mwandishi wetu wa Uganda John Kibego amezungumza na kijana Kento Safari ambaye ni mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, anayejevunia mafanikio yake katika nyanja ya muziki, mipango yake mwakani na pia kuuomba Umoja wa Mataifa kuwapa msaada zaidi. 

Sauti
3'29"
UN SDGs

Vijana waendelea kushiriki katika utimizaji wa SDGs. Zauja Mohamed ni mmoja wao 

Asasi ya Nuru Yetu Foundation chini ya uongozi wa msichana Zauja Mohamed ambaye alianzisha taasisi hii akiwa katika masomo yake ya sekondari miaka michache iliyopita, hivi karibuni imeandaa warsha kwa ajili ya wasichana. Warsha hii imewakutanisha wasichana na baadhi ya watu wenye ushawishi nchini Tanzania ili wasichana hao wapate miongozo mbalimbali ya kuwasaidia kupambana na changamoto za ndani ya jamii kama vile unyanyasaji wa kijinsia, kujikwamua kiuchumi, kielimu na kadhalika.

Sauti
3'39"
FAO/Rudolf Hahn

Mabadiliko ya tabianchi, tishio kwa eneo la bonde la ufa Kenya

Kuongezeka kwa maji kwenye maziwa yaliyo eneo la bonde la ufa nchini Kenya ni jambo ambalo linaendelea kuzua wasiwasi miongoni mwa watu wa maeneo hayo na pia pigo kubwa kwa sekta muhimu ya utalii nchini Kenya. Serikali imekuwa ikiwashauri wale wanaoishi karibu na maeneo hayo kuhama na kujitafutia sehemu salama huku ikitafuta suluhusu ikiwa maji hayo yatazidi kuongezeka siku zinazokuja. Mwandishi wa Kenya Jason Nyakundi amezungumza na mtaalamu wa hali ya hewa nchini Kenya Henry Ndede kutaka kufahamu chanzo ni kipi.

Sauti
2'38"
Warren Bright/UNFPA Tanzania

Waandishi wa habari nao wapata elimu kuhusu SDGs Tanzania

Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam kimewaelimisha waandishi wa habari wa Morogoro Tanzania kuhusu Malengo ya maendeleo endelevu. Kupitia makala hii iliyoandaliwa na Ahimidiwe Olotu, Stella Vuzo wa Kituo hicho cha habari cha Umoja wa Mataifa anaanza kwa kueleza nia ya mafunzo.

Sauti
2'57"