Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Warren Bright/UNFPA Tanzania

Mcheza kwao hutuzwa, Kalah Jeremiah

Shirika la idadi ya watu, UNFPA limewatunukia watu ambao wanapigania usawa wa kijinsi katika jamii nchini Tanzania ambapo msanii wa Hip Hop Kalah Jeremiah amekuwa miongoni mwa watu 16 waliopata tuzo hiyo. Ahimidiwe Olotu wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam amezungumza na msanii huyo. 

 

Sauti
3'10"
UN News/Yasmina Guerda

Mbao ambazo zingetupwa, nazibadili kuwa samani za nyumba

Wanawake wengi duniani, pamoja na sababu nyingine, kutokuwa huru kiuchumi kunawaweka katika hatari ya kunyanyaswa. Catherine Soi wa Kisumu Kenya, amejikwamua na hali hiyo, kwa kubadili mbao ambazo zingetupwa kama asingezibadili kuwa samani za nyumbani. Catherine Soi alitoa ujuzi wake kwenye mitandao wa intaneti na kupitia mtandao wa intaneti ndiko anapatumia sana kufanyia biashara yake. Biashara ya kutengeza fanicha au samani kutokana na mbao zinazotumika kebebea na kuhifadhi mizigo yaani pallets, kazi ambayo imemjenga kiuchumi na kumpa umaarufu wa jina jipya la pallet girl.

Sauti
2'8"

Juhudi za mwanahabari kuchagiza msaada wa kibinadamu Uganda

Kuna msemo unaosema kutoa ni moyo, usemi huu ni dhahiri kwa kuangalia mwanahabari Sophie kutoka Uganda ambaye alikuwa akitumia nafasi yake kuchagiza msaada wa kibinadamu lakini sasa anafanya kwa vitendo. Kutoka kuwa mtanganzaji na sasa ni mhudumu wa kibinadamu, basi ungana na John Kibego katika makala ifuatayo.

Sauti
3'19"
© UNICEF/Amminadab Jean

Siyo ulemavu wote unaonekana-Wataalam wa Afya

Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya kimataifa ya walemavu na kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa “sio ulemavu wote unaonekana” ni bayana kuwa  watu wengi duniani wanaishi na ulemavu wa aina fulani ambao hauonekani ambao wakati mwingine unaweza kuchukuliwa kuwa labda tabia zao na hata watu hao kukumbwa na unyanyapaa katika jamii. Mara nyingi ulemavu unaozingatiwa huwa ule unaonekana kwa mfano ulemavu wa miguu, mikono au macho ingawa nao bado wanakumbana na changamoto nyingi.

Audio Duration
3'46"
© World Bank/Sarah Farhat

Vijana wapeana mawaidha ya kuepuka ghasia mandamanoni, Uganda

Karibu kote duniani vijana hua msitari wa mbele kwneye mandanmano na vilevile kukumbana na matokeo yake ikiwemo vifo, kujeruhiwa na kufungwa jela.

Kawaida sababu ni ukosefu wa ajira na kutaka nafasi kwenye uongozi ingawa mara nyingine baadhi yao hutumikishwa tu bila wao wenyewe kuwa na sababu ya msingi.

Je, ni jinsi gani kijana binafsi yaweza kujizuia kushiriki kwneye mandamano yasio halali na ya ghasia? Je, kwa nini vyombo vya usalama hutumia nguvu kupita kiasi.

Sauti
3'58"
UN Tanzania/Nafisa Didi

Nilitaabika na UKIMWI na sitaki wenzangu wataabike kama mimi- Bi. Masao.

Katika maisha ya binadamu, uzoefu unaonesha kuwa ni nadra kumkuta kiumbe apendaye kuepusha mwenzake kutopitia mabaya yaliyomkumba. Lakini si kwa Hellen Thomas Masao, mwalimu mstaafu nchini Tanzania ambaye anasema kubainika kuwa na Virusi vya Ukimwi, ilikuwa ni kama tiketi ya kifo, lakini mola alimuepusha na sasa anatumia uzoefu wake kuhakikisha walimu wenzake wa umri wake na vijana hawapitii unyanyapaa aliopitia yeye hadi ameanzisha taasisi ya kusaidia walimu wanaoishi na VVU, TAPOTI.

Sauti
5'21"
World Bank / Sarah Farhat

Watoto wa kike Morogoro Tanzania wameitaka jamii kuacha vitendo vya kikatili dhidi yao

Dunia ikiwa katika mfululizo wa siku 16 za kuahamasisha mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia, nchini Tanzania mkoani Morogoro wasichana wamepaza sauti wakionesha kutofurahishwa na ukatili unaofanywa na baadhi ya wazazi na walezi majumbani. Huku wakiiomba serikali kufuata sheria pale mtuhumiwa anapo kamatwa na kufikishwa mahakamani, kwa makosa ya ukatili dhidi ya watoto wa kike. 

Sauti
3'21"
© Julius Mwelu/ UN-Habitat

Mimi mwenyewe nilibakwa, nikaanza kuwasaidia wanawake wengine-Ashura Msiteka

Ulimwengu ukiwa katika siku 16 za kuhamasisha kupinga ukatili wa kijinsia hususani kwa wanawake na wasichana, takwimu zinaonesha kuwa wakati huu wa janga la COVID-19, wanawake wengi zaidi wamedhulumiwa kwa namna moja au nyingine. 

Sasa kikundi cha Coalition of grassroots women initiative kilicho mtaa wa Dandora mjini Nairobi kimekuwa kikiwahudumia wanawake na wasichana ambao wanapitia ukatili wa aina tofauti. Kiongozi wa kikundi hiki Ashura Msiteka ambaye mwenyewe ni manusura wa ukatili  amezungunza na mwandishi wa Kenya Jason Nyakundi kuhusu shughuli zao.

Sauti
3'17"
UN Tanzania/Ahimidiwe Olotu

Wanaume waliona utamu wa kuongoza, wakawaacha dada zao-Getrude Mongela

Ulimwengu ukiwa katika siku 16 za uhamasishaji wa kupinga ukatili dhidi ya wanawake, pamoja na mengine, jamii inakumbushwa kuhusu lengo namba 5 la malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendelepo endelevu, SDGs, lengo ambalo linahamasisha kuhusu usawa wa kijinsia. Lakini jamii za ulimwengu zilifikaje katika kuwa na pengo la usawa wa kijinsia kwa kiasi hiki cha kuwa na uhitaji wa kukumbushwa? Bi.

Sauti
3'21"
UNMISS\Nektarios Markogiannis

Wakati mwingine watu wanafanyiwa vitendo vya ukatili lakini hawajui kuwa huo ni ukatili- Mary Nsia Mangu 

Msichana Mary Nsia Mangu wa Arusha Tanzania, ili kuunga mkono Malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu, SDGs, anaendesha taasisi maalum ya Dexterous Tanzania ambayo ina lengo la kuboresha elimu ya watoto, kuwapatia uelewa kupitia vitabu na pia kuwafahamisha kuhusu ukatili wa kijinsia.  

Vile vile taasisi yake inasaidia kupinga ukatili dhidi ya watoto hususani wa Kike kwa kuwapa elimu kupitia njia mbalimbali ikiwamo kuwafikia moja kwa moja shuleni. Mary anawahamasisha wasichana kuwa majasiri kuleta mabadiliko ndani ya Jamii. 

 

Sauti
2'53"