Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNICEF

Watoto wanasemaje kuhusu mkataba wa kimataifa wa haki za watoto?

Ikiwa leo ulimwengu unaadhimisha siku ya kimataifa ya mtoto,  makala ya Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa inajikita mkoani Morogoro nchini Tanzania ambako watoto wanatoa maoni yao kuhusu siku yao hii na pia mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto, CRC,  ambao umetimiza miaka 30 tangu ulipopitishwa.

Siku ya mtoto duniani ilianzishwa mwaka 1954 na huadhimishwa tarehe 20 mwezi Novemba ya kila mwaka ili kusongesha utangamano na ustawi wa kimataifa miongoni mwa watoto wote duniani.

Sauti
3'13"
MINUSMA/Sylvain Liecht

Hakuna kazi ya mwanaume wala mwanamke ni kujitosa tu:Njeri

Miriam Njeri mshona viatu mashuhuri hivi sasa nchini Kenya, anasema hakutarajia kuwa siku moja angekuja kuwa mshona viatu mkubwa na hata kumiliki kampuni, kazi ambayo kwa kawaida au kwa asililimia kubwa inaminiwa kuwa ya wanaume. Baada ya siku moja kutembelea kazi ya rafiki yake anayemiliki duka la kushona viatu aliamua naye kujitosa katika fani ya ushonaji viatu na kwa sasa amepata mafanio makubwa na kudhihirisha wito wa Umoja wa Mataifa wa kuwachagiza na kuwawezesha wanawake kwa kuwapa fursa .

Sauti
3'31"
USGS/NASA

Asante Benki ya Dunia sasa tunaweza kufungua macho yetu- Wakazi Ningxia, China

Suala la kuenea kwa jangwa ni tatizo ambalo linakumba maeneo mbalimbali duniani kutokana na sababu kadhaa ikiwemo ukataji miti hovyo, ufugaji wa kuhamahama na mabadiliko ya tabianchi. Jamii ndio huathirika zaidi kama ilivyo katika eneo moja huko nchini China ambako jangwa lilienea katika enoe kubwa na hata kusababisha wakazi kupoteza njia za kujipatia kipato, na baya zaidi upepo wa jangwani ukiambatana na vumbi ulikuwa  hatari zaidi kwa macho yao. Hata hivyo Benki ya Dunia ilichukua hatua na kuleta kicheko kwa wakazi wa eneo hilo kama anavyosimulia Grace Kaneiya.

Sauti
3'48"
UN News/Grece Kaneiya

Suala la afya lipo pia mkononi mwako kama mkenya-Waziri Kariuki

Hatua zimepigwa katika kuimarisha afya ya mamilioni ya watu, kuongeza umri wa kuishi, kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua na vita dhidi ya magonjwa yanayoambukiza. Hata hivyo kwa mujibu wa ripoti ya utekelezaji wa lengo namba tatu la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs la  kuhakikisha afya kwa wote, hatua haziendi kwa kasi inayohitajika dhidi ya magonjwa makubwa kama vile malaria na kifua kikuu. Aidha karibu nusu ya watu wote duniani hawafikii huduma muhimu za afya huku wengi wakiteseka kutokana na ukosefu wa fedha.

Sauti
4'10"
UNFPA

Vijana tutumie fursa ili kufanikisha azimio la Cairo kuhudu idadi ya watu na maendeleo- Restless Development

Mwaka 1994 huko mjini Cairo Misri kulifanyika mkutano wa kimataifa kuhusu idadi ya watu na maendeleo, ICPD ambao uliibuka na azimio lenye mambo makuu manne, ambayo ni elimu kwa wote ifikapo mwaka 2015, kupunguza vifo vya watoto wachanga na watoto, kupunguza vifo vya wajawazito na kuhakikisha kuwa huduma za afya ya uzazi ikiwemo uzazi wa mpango zinapatikana kwa watu wote ikiwemo vijana wa kike na wa kiume.

Sauti
3'52"
FAO

Umuhimu wa nyuki kwa mazingira na kipato wangaziwa, Uganda

Nyuki wana mchango mkubwa katika maisha ya binadamu na mazingira na hasa umaarufu wake wa kuzalisha chakula kisichooza ambacho ni asali. Lakini manufaa ya nyuki yanaenda mbali zaidi ya asali hadi kwneye uzalishaji wa vyakula mbalimbali vya kawadia , dawa na pia utunzaji wa mazingira kwani nyuki ni sehemu muhimu ya ukuaji uendelevu wa mimea. Lakini sasa wadudu hao wako hatarini kutokana na  uchafuzi na uharibifu wa misitu na mazingira kwa ujumla ambayo ni maskani yao, yakiripotiwa kuwa changamoto duniani kote.

Sauti
3'49"
UN/Sawiche Wamunza

Mradi wa UN na Tanzania wapeleka furaha kwa wanakijiji wa Magunga mkoani Tanga

Mwezi  uliopita wa Oktoba, wakazi wa kijiji cha Magunda, wilaya  ya Korogwe mkoani Tanga nchini Tanzania waligubikwa na furaha isiyo kifani baada ya kushuhudia mashamba yao yakigeuka kuwa kitegauchumi na mtaji kwa ajili ya kuboresha maisha yao. Hii ni baada ya Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la mpango wa maendeleo UNDP na mfuko wa mazingira duniani, GEF na serikali yenyewe ya Tanzania kufanikisha mradi wa kugawa hati 250 za kumiliki ardhi.

Sauti
4'16"
UN/Assumpta Massoi

Tukifanikiwa kuondoa pengo kati ya wanawake na wanaume tutakuwa na jamii endelevu-Kijana Koka

Suala la ajira kwa vijana ni changamoto katika nchi nyingi na sasa hivi kuna wito wa kubadili hali ambapo vijana wenyewe wamechukua jukumu la kujiajiri wenyewe au kufanya kazi za kujitolea. Mmoja wa vijana hao ni kutoka nchini Tanzania amabaye yeye licha ya kwamba amekwenda chuo kikuu na kuhitimu shahada ya uzamili na kuwa wakili, sasa anafanya kazi ya kutjitolea katika shirika la kiraia la Restless development nchini humo. Kulikoni? Ungana na Grace Kaneiya katika makala hii akizungumza na kijana huyo ambaye anaanza kwa kujitambulisha.

Sauti
5'44"
UNHCR/Benjamin

Mtazamo wa wazee kwa ndoa za utotoni huko Turkana

Ndoa za mapema ni jinamizi lililojikita mizizi katika tamaduni mbalimbali hasa zile za wafugaji barani Afrika, zikiathiri vibaya ustawi wa watoto wa kike. Jamii hizo ni pamoja na Karamajong Kaskazini Mashairki mwa Uganda, Toposa wa Kusini mashariki mwa Sudani Kusini nan a Masai na Turkana nchini Kenya.

Katika jamii ya Turkana Kenya, ndoa hizo ni sehemu ya utamaduni wao na unaathiri vibaya ustawi wa watoto wa kike kama vile kushindwa kupata elimu na hata madhara kwenye afya ya uzazi pindi wanapobeba ujauzito katika umri mdogo.

Sauti
3'57"