Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UN/maktaba

Ndoto yangu imetimia, nitajitahidi kwa kadri ya uwezo wangu- Mtoto Rehema

Hatimaye mtoto Rehema Paul ambaye aliponea chupuchupu kuajiriwa kazi za ndani baada ya mwajiri wake kubaini kuwa umri wake  haukuwa unaruhusu kufanya kazi, sasa ameanza masomo katika shule ya msingi Mchikichini, kwenye manispaa ya Morogoro nchini Tanzania. Mwajiri huyo, Herieth Mkaanga amefurahi sana kwani amefanikisha lengo namba 4 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs la kutaka elimu kwa watoto bila ubaguzi wowote ule na wakati huo huo kufanikisha ndoto ya mtoto Rehema ya kupata elimu.

Sauti
4'24"
UN

Natumia uelewa wangu kuhusu mauaji ya halaiki kuepusha yasiyotokee tena- Mwanafunzi Tanzania

Miaka 74 tangu kukombolewa kwa kambi ya mateso na mauaji ya wayahudi milioni Sita huko  Auschwitz-Birkenau, nchini Poland yaliyofanywa na manazi wa Ujerumani, bado kuna ubaguzi kwa misingi mbalimbali iwe ya kidini au kikabila. Hali hii  hutia sana wasiwasi Umoja wa Mataifa ambao uliamua siyo tu kutenga siku ya kimataifa ya kumbukizi ya mauaji hayo ya halaiki dhidi ya wayahudi kama fursa ya kukumbuka na kutathmini, bali pia kuwa na programu maalum ya kuelimisha jamii juu ya madhila ya mauaji ya aina hiyo na viashiria vyake ili kuepusha yasitokee tena.

Sauti
4'5"
UNEP GRID Arendal/Peter Prokosch

Maarifa ya jamii za asili huziwezesha kuishi vyema na wanyamapori

Watu wa jamii za asili mara kwa mara wameelezea wasiwasi wao kuhusu juhudi za kuhifadhi mazingira kutozingatia haki na maarifa ya kundi hilo. Jamii hiyo hutolea mifano harakati za kutengwaa maeneo ya uhifadhi ambapo inasema kuwa husababisha watu hao kufurushwa makwao na hata kupoteza kipato. Changamoto hiyo iliangaziwa kwenye ripoti ya mwaka 2016 ya mtaalam huru wa haki za watu wa asili na ilijadiliwa mwaka 2018 katika kikao cha kudumu cha watu wa asili.

Sauti
4'7"
World Bank/Charlotte Kesl

Ubunifu wa ajira wazaa matunda kwa vijana nchini Burundi

Kubuni ajira ni swala linalotatiza pakubwa vijana wengi barani Afrika. Wengi hulalamikia ukosefu wa mitaji au chanzo cha kuanzisha biashara. Lakini wataalamu wa biashara na wachanganuzi wa miradi  wanaamini kuwa mtaji mkubwa na wa kuaminika kwanza ni  fikra ya biashara  pamoja na kujumuika katika shirika.

Kundi moja la vijana wapatao 50 nchini Burundi  kwa jina la CVC, baada ya kupokea  mafunzo ya mtaalamu wameanza kuona mafaanikio  ya biashara yao ilioanza  tu na unga wa uji.

Sauti
3'52"
Photo: IRIN/Mujahid Safodien

Taasisi ya PGWOCADE na harakati za kumkomboa msichana mkoani Rukwa Tanzania.

Mojawapo ya vikwazo vya harakati za kumwinua mwanamke kutoka katika hali duni iliyodumu tangu enzi na enzi mila na desturi za baadhi ya maeneo duniani ambayo wanajamii wamekwenda kwa kasi ndogo katika kuziacha mila hizo kandamizi na potofu. Licha ya ugumu huo, bado mazingira hayo hayapaswi kuwa kikwazo kwa wanarahakati ambao wanahaha kufikia  usawa wa kijinsia kwani mabadiliko ya mila na desturi hayawezi kuwa ya siku moja.

Sauti
4'27"
IOM/Amanda Nero

Wakazi wachukua hatua kulinda mto Nkumara Uganda

Maziwa, hifadhi za maji na mito vyote vina umuhimu mkubwa si tu kwa mazingira bali pia binadamu wanaozingira vyanzo hivyo vya maji. hata hivyo licha ya vyanzo hivi kuwa na umuhimu mkubwa kiuchumi, kimazingira na kiutamaduni bado vinakabiliwa na athari kutokana na shughuli za binadamu ambazo zinaweza kusababisha uharibifu wa vyanzo hivyo. Ulinzi kutokana na shuhguli hizo ni muhimu na ni kwa mantiki hiyo ambapo wakazi wa mto Nkumara nchini Uganda ambao wamechukua hatua kuandika katiba katika kuhakikisha ulinzi wa mto huo. Je kulikoni?

Sauti
3'57"
UN /MINUSCA

Kijana mkimbizi atumia radio chakavu kurusha matangazo huko kambini Kyangwali nchini Uganda

Leo Ijumaa katika makala kwa kina tuko nchini Uganda katika kambi ya wakimbizi ya Kyangwali, ambako John Safari, mkimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), ametumia ubunifu na ujuzi wa kukarabati redio na kuanzisha mtambo wa kurusha matangazo ya  redio yanachohabarisha jamii ya wakimbizi katika kambi ya Kyangwali nchini Uganda. Ungana na John Kibego katika mahojiano na mbunifu huyo.

Sauti
5'12"