Uvumbuzi wa mashine ya kukausha nafaka ni habari njema kwa mkulima Thika, Kenya
Wakulima wengi hukumbwa na changamoto za kuhifadhi mazao yao baada ya kuyavuna hususan nafaka hali inayawaletea hasara kubwa ya kupoteza chakula na hali kadhalika kusababishia familia zao taabu kama vile ukosefu wa chakula. Sasa mkulima mmoja nchini Kenya David Burii, amebuni kifaa kinachowasaidia wakulima kukausha nafaka yao kwa njia rahisi. Mwandishi wetu kutoka Kenya Jason Nyakundi alimtembelea kwenye karakana yako huko Thika na kututumia ripoti hii.