Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

UNEP

Hofu yatanda juu ya uchafuzi wa Msitu Bugoma, Uganda

Kwa mujibu wa shirika la mpango wa mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP misitu ni rasilimali adhimu katika suala zima la uhifadhi wa mazingira na kudhibiti mabadiliko ya tabianchi. Pia hua ni msingi wa maisha na kipato kwa kuwezesha kilimo na upatikanaji wa nishati kwa asilimia kubwa ya watu dunaini hasa wale waishiyo katika maeneo ya vijijini. Matumizi endelevu ya rasilimali asili kwa maslahi ya mazingira limeaorodheshwa katika malengoya maendeleo endelevu au SDGs.

Sauti
3'42"
UN News/Conor Lennon

Kampeni ya mmoja kwa mmoja kusaidia kufanikisha SDGs

Wiki hii viongozi wa Umoja wa Mataifa wamepitisha azimio la kisiasa la huduma ya afya kwa wote ikilenga kuhakikisha kuwa huduma hiyo inapatikana kwa kila mkazi wa dunia hii ifikapo mwaka 2030. Kando mwa azimio hilo kumefanyika vikao vya kando vikileta wadau wa shirika la afya  ulimwenguni, WHO kujadili na kutathmini mwelekeo wa malengo ya afya na ustawi kwa wakazi wa dunia na  miongoni mwa ni Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya kikwete ambaye ni mwanzilishi wa kampeni ya One By One Target 2030 au mmoja mmoja ifikapo mwaka 2030.

Sauti
2'41"
© UNICEF/Arjen van de Merwe

EAGT na harakati za kutunza afya ya vijana

Wiki hii kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kumefanyika mkutano wa ngazi ya  juu wa viongozi sambamba na vikao vya kando kuchagiza afya kwa wote kama jawabu la kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Suala la afya kwa wote linapigiwa sasa chepuo na vijana wenyewe kupitia programu mbalimbal iikiwemo ile ya kuibua vipaji miongoni mwa nchi za Afrika Mashariki, EAGT inayoendelea hivi sasa kwenye ukanda huo.

Sauti
3'56"
UN News/Grece Kaneiya

Jamii na serikali wanaitikia wito wa huduma za uzazi wa mpango

Vikao vya ngazi ya juu vya Umoja wa Mataifa vikiendelea kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani, mashirika ya kiraia nayo yanashiriki katika vikao vya kando kuelezea kile ambacho yanafanya mashinani kuchagiza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs huko mashinani. Miongoni mwa mashirika  hayo ni lile la Restless Development nchini Tanzania ambalo kupitia mradi wa Tutimize ahadi linasaka takwimu kuangazia ni jinsi gani serikali inatekeleza ahadi za usawa wa kijinsia na mkakati wa uzazi wa mpango wa mwaka 2020.

Sauti
4'11"
© UNICEF/Pirozzi

Kutowaacha nyuma watoto wenye ulemavu ni kutimza mahitaji yao

Elimu kwa wote ni moja ya malengo ya maendeleo endelevu au SDGs ambalo linasisitiza usawa baina ya watoto wa kike na wa kiume katika kupata elimu bora lakini pia watoto wenye mahitaji maalum. Mkoani Songwe nchini Tanzania kuna shule ya watoto wenye mahitaji maalum lakini pamoja na kusoma kwenye shule maalum kuna changamoto lukuki zinazowakabili watoto hao ikiwemo miundombinu, vifaa na hata masuala ya msingi kama maji. John Kabambala kutoka Radio washirika TanzaniaKidsTime FM ametembelea shule hiyo kujionea hali halisi na kuzungumza na walimu na wanafunzi.

Sauti
3'43"
UN Environment

Miradi ya UNFPA imetuletea nuru katika maisha yetu hapa Zanzibar-Asia Rashid

UNFPA ikiadhimisha miaka 25 ya kongamano la idadi ya watu  na maendeleo ICPD25 ambapo lengo ni pamoja na kutokomeza vifo vya mama na mtoto, kuhakikisha mahitaji yote ya uzazi wa mpango yanawafikia wahitaji na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto  kufikia mwaka 2030, imeendelea kutathmini  mafanikio ya miradi mbalimbali ambayo imeshatekelezwa kote duniani ikiwemo Tanzania bara na visiwani.

Sauti
3'23"
UN Environment

UN Environment na maandalizi kuelekea mkutano wa hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi

Kuelekea mkutano wa hatua dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi utakaofanyika hapa jijini New York, Marekani mnamo Septemba 23 mwaka huu, watu, serikali na mashirika wamekuwa wakifanya maandalizi yatakoyofanikisha mkutano wa Katibu Mkuu wenye lengo ya kuchagiza nchi kuchukua hatua kwa pamoja kukbailiana na changamoto ya mabadiliko ya tabianchi.

Sauti
3'52"
World Bank/Arne Hoel

Mikakati ya kuhakikisha uhakika wa chakula yangaziwa, Uganda

Lengo la pilli katika Malengo ya Maendeleo Endelevu au SDGs linachagiza kilimo endelevu ili kuhakikisha uhakika wa chakula na lishe ambapo serikali zimekuwa zikichukua hatua mbalimbali  kuhakikisha lengo hilo linatimizwa ambalo ni msingi wa utekelezaji wa amlengo mengine hasa utokomezwaji wa umaskini.

Miongoni mwa mbinu zinazochukuliwa nchini Uganda ni usambazaji wa mbegu bila malipo kwa wanchi mbegu ambazo serikali inaamini kuwa ni bora kuliko zile za asili.

Sauti
4'3"