Mchango wa wakunga wa jadi ni dhahiri hususan, Mwanza-Tanzania
Katika mfululizo wa makala zetu tukiangazia wakunga na wauguzi mwezi wa Februari, Leo tunaelekea mkoani Mwanza nchini Tanzania ambapo redio washirika, Redio SAUT, iliyoko mkoani Mwanza nchini Tanzania, katika makala iliyoandaliwa na Evarist Mapesa na kusimuliwa na Nyota Simba, inaangazia mkunga wa jadi Emmy Paulo Chalamila wa zahanati ya Igogo ya jijini Mwanza, Tanzania.