Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala ya Wiki

UN News/ John Kibego

Changamoto zitokanazo na ugonjwa wa kisukari

Tukielekea siku ya kisukari duniani hapo kesho shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO linasema idadi ya wagonjwa wa kisukari duniani inaongezeka na ugonjwa huo unakatili maisha ya watu…. Kila mwaka. Ndio maana mwaka huu kaulimbiu ni waauguzi na kisukari ikiwa ni kampeni ya kuelimisha kuhusu umuhimu wa jukumu la watu hao katika vita dhidi ya kisukari.  Hata hivyo unapokuwa mkimbizi katika mkambini au makazi ya wakimbizi ukitegemea msaada kuweza kuishi kisukari ni msumari wa moto juu ya kidonda.

Sauti
7'12"
Video screenshot/Loise Wairimu

Kutoka Kenya hadi Marekani kupata mafunzo kwa vitendo

Loise Wairimu, ni msichana ambaye alifunga safari kutoka Kenya kuja hapa jijini New York Marekani katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa ili apate mafunzo kwa vitendo.

Kwa takribani kipindi cha miezi sita amefanya kazi pamoja na timu nzima ya Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa akichota maarifa ya kazi. Loise anaanza kwa kueleza namna safari yake hii ilivyoanza na alichojifunza mchakato huu.

Sauti
6'4"
UN / Anton Uspensky

Umoja wa Mataifa ukitimiza miaka 75 na mafanikio iliyoyafikia

Kesho ni siku ya Umoja wa Mataifa, chombo hicho kikitimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake! Katika mada kwa kina Anold Kayanda anatupitisha safari ya kuanzishwa kwake na zaidi ya yote simulizi ya mtu aliyezaliwa mwaka mmoja na Umoja wa Mataifa, mtu ambaye amewahi kushika nyadhifa ndani ya Umoja wa Mataifa, barani Afrika na ndani ya taifa lake la Tanzania. Kwako Anold!

Sauti
5'24"
WHO/P. Virot

Watu bilioni 1 duniani wanaishi na matatizo ya akili-Takwimu

Kuelekea siku ya afya ya akili duniani itakayoadhimishwa kesho Jumamosi Oktoba 10, takwimu zinaonesha kuwa takribani watu bilioni 1 duniani kote wanaishi na matatizo ya akili. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake kwa siku hii amesema, inabidi hatua zichukuliwe ili kuhakikisha kunakuwa na huduma bora ya afya ya akili kwa wote kwani hivi sasa inaonesha pia kuwa kila sekunde 30 mtu mmoja anajiua kutokana na tatizo hili la afya ya akili. 

Sauti
5'42"
© Julius Mwelu/ UN-Habitat

Mapambano dhidi ya COVID-19 Kenya

Watu waliopoteza maisha hadi sasa kote duniani kutokana na virusi vya corona ikiwa imevuka 20,000 huku zaidi ya watu nusu milioni kote duniani wakiambukizwa virusi hivyo hatari nchini Kenya kama zilivyo nchi nyingine, mapambano dhidi ya ugonjwa huo yanaendelea. Katika makala ya leo, mwandishi wetu wa Nairobi Jason Nyakundi anaangazia tahadhari ambazo watu wa Kenya wanazichukua kujikinga na virusi vya corona na changamoto wanazokumbana nazo.

Sauti
6'6"
UN News/ John Kibego

Hisia za wakimbizi nchini Uganda kufuatia mlipuko wa Corona unaoshuhudiwa duniani kote

Katika makala ya wiki hii tutakuwa nchini Uganda tukiangazia shaka na shuku miongoni mwa wakimbizi na hatua za Umoja wa Mataifa wakati huu wa maambukizi ya Corona.  

Mwandishi wetu wa Uganda, John Kibego alikwenda kambi ya wakimbizi ya Kyangwali kusikiliza shaka na shuku zao kuhusu hofu ya kuingia kwa virusi vya corona kwenye taifa hilo ambalo bado halina mgonjwa hadi leo Ijumaa. 

Sauti
4'56"