Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala ya Wiki

Unsplash/Drew Willson

Ni lazima wanawake tujiamini – Fundi viatu Jovia Kyomuhendo

Ubunifu ni moja ya mambo yanayotazamwa kuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu, SDGs. Nchini Uganda, msichana Jovia Kyomuhendo amepata sifa kwa kuwa kijana mbunifu ambaye amefikia hatua ya kujiajiri kwa kuanzisha kiwanda kidogo cha kushona na pia kutengeneza viatu.

Safari yake imekuwaje hadi kufikia kutunukiwa tuzo na Muungano wa Viwanda Vidovidogo nchini Uganda USSIA? Tupate taarifa zaidi kutoka kwa mwandishi wetu wa Uganda, John Kibego.

Sauti
3'41"
UN News/Devotha Songorwa

COVID-19 imekuwa mwiba kwa wavuvi mkoani Kigoma Tanzania

Janga la corona au COVID-19 limeendelea kuitikisa dunia kijamii na kiuchumi karibu kila pembe ya ulimwengu. Na hali ndivyo ilivyo kwa wavuvi wa ziwa Tanganyika mkoani Kigoma ambako Devotha Songorwa kutoka Radio washirika TanzaniakidsTime FM amezungumza na wavuvi mbalimbali wa ziwa Tanganyika mkoani huo kutaka kujua je wanafahamu nini kuhusu janga hili , limewathiri vipi, na endapo wanatambua kuhusu suala la chanjo  na umuhimu wake katika kuwanusuru wavuvi na sekta hiyo wakati huu wa janga la COVID-19? Ungana nao katika Makala hii.

 

Sauti
5'37"
UNAMA/Eric Kanalstein

Mradi wa Mfereji wa Maji waboresha maisha ya wakazi wa Kabul, Afghanistan

Kila siku wananchi watano katika kijiji cha Pazhaki jimboni Kabul nchini Afghanisan walikuwa wanajukumu la kufungulia maji katika mfereji uliokuwa unategemewa na wanakijiji hao kwa shughuli za kilimo. Lakini Ramazan Ibrahimkil, mwenyekiti wa Kijiji cha Pazhak anasema alikuwa anapokea kesi kila uchwao kwamba wananchi wanaokaa milimani wakilalamikiwa kufungulia maji kwa wingi na hivyo wale wa mabondeni kukosa maji ya kutosha kwenye kilimo chao na hivyo kupata mazao machache na kipato kidogo. 

Sauti
4'41"