Umoja wa Mataifa na usaidizi nchini Burundi kwa mwaka huu wa 2016
Katika mfululizo wa makala za kuangazia kazi za Umoja wa Mataifa katika ukanda wa nchi za maziwa makuu, tumejikita Burundi nchi ambayo mwaka jana ilikumbwa na sintofahamu ya kisiasa kabla na baada ya uchaguzi mkuu.
Umoja wa Mataifa kupitia Baraza la Usalama, na wawakilishi wake walifanya kazi ngumu ya kusaka suluhu ya kisiasa baada ya Rais wa nchi hiyo Piere Nkurunzinza kugombea mhula wa tatu wa Urais licha ya utata wa katiba, hatua iliyozua tafrani katika taifa hilo la kwani upinzani ulisusuia uchaguzi ukipinga hatua hiyo na hivyo kuzua machafuko.