27 DESEMBA 2023
Hii leo jarida linajikita barani Afrika likianzia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kuangazia uchaguzi, wapiganaji wa zamani na MONUSCO, halikdhalika Jiko Point na mashinani ni nchini Kenya.
Hii leo jarida linajikita barani Afrika likianzia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kuangazia uchaguzi, wapiganaji wa zamani na MONUSCO, halikdhalika Jiko Point na mashinani ni nchini Kenya.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kazi ya kuhesabu kura inaendelea baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Jumatano na kuendelea katika baadhi ya maeneo jana Alhamisi, huku ikielezwa kwamba jimboni Ituri, maisha yamerejea katika hali ya kawaida kwenye eneo la Fataki baada ya mwaka mmoja wa mashambulizi kutoka kwa wanamgambo waliojihami wa kundi la CODECO.
Njaa imeukumba Ukanda wa Gaza kwa mujibu wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO na hivyo kutishia ongezeko la magonjwa hususan miongoni mwa watoto, kina mama wajawazito na wanaonyonyesha na makundi mengine yaliyo hatarini na nishati ya kupikia nayo imeota mbawa.
DAFI, Mfuko wa Ufadhili wa Kimasomo kwa Wakimbizi, kwa kushirikiana na UNHCR wanawasaidia wakimbizi kutimiza ndoto zao za kupata elimu ya juu katika nchi ya kwanza wanakopata hifadhi baada ya kuzikimbia nchi zao.
Idadi ya waliokwisha kunufaika na ufadhili wa DAFI inazidi kuongezeka lakini takwimu za hivi karibuni zinaonesha angalau hadi kufikia mwaka jana 2022 DAFI ilipotimiza miaka 30 tangu kuanziswa kwake, chini ya serikali ya Ujerumani na wadau wengine, tayari imewafadhili wakimbizi zaidi ya 24,000 kusoma elimu za juu iwe vyuo vikuu au vyuo vingine vya ujuzi.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linahimiza kila nchi kuhakikisha watoto wote wenye umri wa chini ya miaka 5 wanapatiwa chanjo dhidi ya polio ugonjwa ambao sio tu unasababisha ulemavu kwa watoto lakini pia ukakatili maisha yao. Kwa msaada kutoka wakfu wa Bill na Melinda gates hivi karibuni UNICEF na shirika la afya duniani WHO nchini Tanzania walizindua kampeni kubwa ya chanjo dhidi ya ugonjwa huo iliyowafikia watoto zaidi ya milioni 4.
Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, uchaguzi mkuu wa Rais, Magavana, wabunge na madiwani umefanyika hii leo kama ilivyopangwa licha ya changamoto zilizojitokeza katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo.
Nchini Tanzania shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kwa kushirikiana na wadau wamewezesha kaya zinazopakana na kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu mkoani Kigoma kujitengenezea mkaa mbadala na hivyo kusaidia kupunguza uharibifu wa mazingira unaosababishwa na ukataji miti kwa ajili ya mkaa.
Hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbayá katika Ukanda wa Gaza Mashariki ya Kati, huku hospitali zilizosalia zikiendelea kushambuliwa na kukatili maisha ya watu na kufungwa kwa mawasiliano ya simu na mtandao wa intanet vikizidisha adha yameonya leo mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Baada ya Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kuitambua lugha ya Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha za kimataifa, sasa Tanzania imetangaza kwamba kwa kushirikiana na nchi nyingine wataanza kutoa Tuzo za Kimataifa za Kiswahili. Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo wa Tanzania Dkt. Damas Ndumbaro amemweleza hayo mwandishi wa Idhaa hii Leah Mushi aliyehudhuria ufunguzi wa Kongamano la nane la Kimataifa la Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani (CHAUKIDU), uliofanyika leo jijini Arusha kaskazini mwa Tanzania.
Mashirika ya umoja wa Mataifa lile mazingira duniani UNEP na lile la afya WHO nchini Kenya yamehimiza umuhimu wa kuhakikisha mazingira safi kwa ajili ya afya bora katika kampeni maalum iliyofanyika jana Alhamisi walipowaalika wanaridha kadhaa wa Kenya kwenye ofisi za Umoja wa mataifa jijini Nairobi. Lengo ni kuzungumza na wanariadha hao kuhusu uhusiano uliopo baina ya mazingira na afya bora ili watambue na kuwa msitari wa mbele kuchagiza hilo katika tasnia yao ambayo mara nyingi hufanyika katika maeneo ya wazi na hewa safi ni muhimu.