Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

WHO Video

Hospitali zazidi kuzidiwa uwezo, wagonjwa sakafuni katika hospitali - Mzozo Gaza

Ikiwa leo ni siku ya 93 tangu mapigano yaanze huko Ukanda wa Gaza kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wa kipalestina waliojihami, likiwemo kundi la Hamas, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya usaidizi wa kiutu yanazungumzia uwepo wa idadi kubwa ya vifo miongoni mwa wanawake na watoto huku yakisihi timu za madaktari ziruhusiwe kuingia eneo la Gaza ili ziendelee na jukumu la kuokoa maisha.  

Sauti
2'16"
OCHA/ Trond Jensen

Wananchi wa jimboni Anambra, Nigeria wapata bima ya afya kwa bei nafuu kwa usaidizi wa WHO

Nchini Nigeria katika Jimbo la Anambra shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya Afrika kwakushirikiana na mpango wa Bima ya Afya ya Serikali wanabadilisha maisha ya wananchi kwa kulipia sehemu kubwa ya gharama za matibabu ili kuhakikisha kila mtu anaweza kupata huduma za afya bila kudumbukia katika umaskini. 

Sauti
2'9"
© UNICEF/Abed Zagout

Uwasilishaji misaada kaskazini mwa Gaza umezuiliwa na vizingiti vya kufikisha misaada ya kibinadamu

Wasaidizi wa kibinadamu wanatoa wito wa fursa ya ufikishaji misaada kwa haraka, salama, endelevu na usiozuiliwa kaskazini mwa Gaza kwani hali ya binadamu inazidi kuwa tete. 

Umoja wa Mataifa na wadau wengine wa misaada ya kibinadamu wameshindwa kutoa msaada unaohitajika haraka wa kuokoa maisha kaskazini mwa Wadi Gaza kwa siku nne kutokana na ucheleweshaji na kukataliwa, pamoja na migogoro inayoendelea imeeleza Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya dharura OCHA katika taarifa yake iliyokusanya takwimu za hadi jana Jan 4 na kuchapishwa leo Jan 5.  

Sauti
1'50"
© UNICEF/Josh Estey

Si haki kutumia gesi ya Nitrojeni Hypoxia kumuua Kenneth - Wasema wataalam wa UN

Wataalamu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa akiwemo Alice Jill Edwards, anayeshughulikia masuala yanayohusu mateso, na Adhabu nyingine za Kikatili, za kinyume cha utu au za Kushusha hadhi, leo Januari 3 mjini Geneva-Uswisi wameelezea wasiwasi wao kuhusu kukaribia kutekelezwa kwa hukumu ya kifo kwa kutumia gesi ya nitrojeni hypoxia dhidi ya Kenneth Eugene Smith hapa nchini Marekani. Mwenzangu Anold Kayanda amekifuatilia kisa hicho kwa kina… 

Sauti
2'1"
© IMF

UN yasema inashikamana na Japan wakati huu taifa hilo limekumbwa na tetemeko kubwa la ardhi

Harakati zikiendelea za kunasua watu waliokwama kwenye vifusi kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililokumba eneo la kati mwa Japan Jumatatu alasiri kwa saa za huko na kusababisha vifo vya watu 62, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameelezea masikitiko yake kufuatia tetemeko hilo lililokuwa na ukubwa wa 7.6 katika kipimo cha Richa. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi

Sauti
1'36"
UN/Michael Ali

DRC: Asante MONUSCO kwa kuniepusha kuwa mpiganaji msituni

Bila MONUSCO ningalikuwa bado msituni – Mpiganaji wa zamani DRC

Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, kazi ya kuhesabu kura za Rais kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 20 na kuendelea katika maeneo mengine siku zilizofuata, inaendelea huku nao wanufaka wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO ambao umeanza kufunga virago, wakitoa shukrani zao. Ufafanuzi zaidi anakupataia Anold Kayanda.

Sauti
1'31"